• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YA MOROGORO YAKUTANA NA WADAU KUJADILI FURSA ZA UWEKEZAJI

Posted on: October 30th, 2019

Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro imekutana na wadau mbalimbali wa sekta ya umma na binafsi kwa lengo la kujadili taarifa iliyoandaliwa na mtaalamu mwezeshaji kutoka shirika la FOSEWERD Initiative Limited ya Jijini Dodoma kwa kushirikiana na wataalamu wa manispaa h iliyoainisha fursa za uwekezaji zilizopo katika Manispaa ya Morogoro.

Akifungua kikao hicho cha majadiliano Meya wa Manispaa ya Morogoro Pascal Kihanga alisema kuwa katika taarifa hiyo imetajwa mikakati ya kuvutia wawekezaji, jinsi gani ya kuzinadi fursa za uwekezaji, changamoto za uwekezaji na pia imetoa mapendekezo ya namna gani ya kutatua changamoto ili kuchochea ukuaji wa biashara na uwekezaji katika manispaa.

Meya Kihanga alisema kuwa Serikali inawajibu wa kushirikiana na sekta binafsi kufanikisha azma ya kujenga uchumi imara wa Halmashauri, mkoa na nchi kwa ujumla.

Aidha Kihanga alisema kuwa Serikali inawajibu mkubwa wa kuhakikisha inaboresha mazingira rafiki na wezeshi ya kufanya biashara na uwekezaji kwa ujumla ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba miundombinu ikiwemo ya mawasiliano, usafirishaji na nishati inakuwa bora.

Pia Serikali inawajibu wa kufanya marekebisho ya kanuni ama sheria ndogo zinazotajwa kuwa ni vikwazo kwa uwekezaji au uendeshaji biashara na kutoa mrejesho wa marekebisho ya kanuni na sheria hizo kwa wawekezaji.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chemba ya wafanyabiashara, wenye viwanda na wakulima TTCIA Mwadhin Myanza alisema kuwa taarifa hiyo ya fusra za uwekezaji itasaidia kuweka mikakati mizuri ya uwekezaji kwa kuwa imetaja maeneo ya uwekezaji, aina za uwekezaji na namna ya kukabiliana na changamoto za uwekezaji.

Hata hivyo Myanza alisema kuwa TCCIA imeweka kipaumbele katika kuhimiza utoaji wa huduma za pamoja (One stop center) ili kuondoa usumbufu kwa wafanyabishara ambao wamekuwa wakisumbuka kupata huduma za kibiashara zikiwemo za TRA.

Naye meneja masoko wa kiwanda cha kubangua mpunga cha MW cha Morogoro Matha David alisema kuwa midahalo na majadiliano yanayohusu uwekezaji yamekuwa yakisaidia kupunguza changamoto mbalimbali zinazokwaza kwenye uwekezaji.

Kuhusu Changamoto Matha alisema awali umeme ulikuwa ukikatikakatika lakini kwa sasa tangu wameanza uzalishaji tatizo hilo limekwisha na pale inapotokea hitirafu Tanesco wamekuwa wakitoa taarifa kabla hawajakata umeme hata hivyo alitaja changamoto ya maji kuwa bado inakwaza wawekezaji wengi hasa wale ambao bidhaa wanazozalisha zinatumia maji.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa