• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YA MOROGORO YAKUTANISHA WADAU WA MAENDELEO KWENYE MDAHALO WA KUJADILI UKUSANYAJI WA MAONI YA DIRA YA MAENDELEO YA TAIFA 2025-2050

Posted on: July 24th, 2024

MANISPAA ya Morogoro imekutanisha wadau mbalimbali wa maendeleo kwenye mdahalo wa ukusanyaji wa maoni ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025-2050 uliofanyika Ukumbi wa Ofisi Kuu ya Manispaa Julai 23-2024.

Imeelezwa kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 imeweza kwa kiasi kikubwa kusogeza mbele maendeleo ya nchi katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, huduma za afya, miundombinu, maji pamoja na maendeleo ya kiuchumi licha ya changamoto mbalimbali ikiwemo Covid 19 ambayo imesababisha kuchelewa kwa baadhi ya mipango.

Katika ufunguzi wa mdahalo huo Ndg.Hillary Sagara , ambae alimwakirisha Mkuu wa Wilaya ya  Morogoro, Mhe. Rebeca Nsemwa, amesisitiza Viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Morogoro  walioshiriki kikao hicho kushirikisha wadau mbalimbali kwenye mchakato wa maandalizi ya Dira hiyo ili kupata maoni yatakayo isaidia nchi katika kukua zaidi kiuchumi.

Naye mwenyekiti wa mdahalo huo Ndg.Bakari Msulwa, amesema Dira ya Maendeleo 2025 ilianza kutekelezwa mwaka 2000 na utekelezaji wake utakamilika 2025 na tunatarajia kuanza kutekeleza Dira nyingine ya mwaka 2025-2050 lengo likiwa ni kuiwezesha nchi kuingia katika kundi la nchi za uchumi wa kati.

Aidha ameeleza kuwa kwa ushirikishwaji mpana wa wadau mbalimbali katika maandalizi ya Dira ya maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025-20250 utawezesha kupata Dira jumuishi yenye kukidhi mahitaji stahiki ya Taifa kwa kipindi cha miaka 25 ijayo.

Amesema, Dira ya 2025  pia ilitazamia kuwa na Taifa lenye sifa kuu tano ambazo ni Maisha bora na mazuri,kuwepo kwa amani,utulivu na umoja,uongozi bora na utawala wa kisheria,jamii iliyoelimika na inayopenda kujifunza Zaidi na uchumi imara wenye uwezo wa ushindani ili kukabiliana na nchi nyingine.

Pia, Msulwa, ameongeza kuwa dira ya maendeleo ya Taifa ina gusa makundi yote, hivyo anatarajia ushirikishwaji mpana wa wadau wote katika ngazi zote zikiwemo taasisi za elimu, sekta binafsi, asasi za kiraia na mwananchi mmoja mmoja.

“ Lengo la kujadili mpango wa maendeleo ya dira ya Taifa ya miaka 25 iliyopita na miaka 25 ijayo ni  kuimarisha uwezo wa uchumi uliopo na kulinda mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025” Amesema Msulwa.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga, amesema kwa kushirikiana na Baraza la Madiwani na Menejimenti ya Manispaa ya Morogoro watahakikisha kuwa wanatoa elimu kwa wafanyakazi pamoja na wa wanafunzi wa Chuo vyuo ili waweze kutoa maoni kuhusu Dira ya taifa 2050.

Kihanga,amesema kuwa , Dira ya maendeleo 2025 imeisaidia sekta ya elimu kukuwa ikiwemo upatikanaji wa mikopo kwa vyuo vya kati ambayo imewasaidia wanafunzi kujiendeleza kielimu na kuwaondolea wazazi mzigo wa ada kwa watoto wao.

Kwa upande wa mshiriki, Rubben Rashid, amesema  miaka 25 ijayo ya mpango wa maendeleo, Serikali ijikite katika utoaji wa elimu yenye kumfanya mwanafunzi kujiajiri badala ya kuajiriwa.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha CHAUMA Manispaa ya Morogoro, Ismail Rashid, amesema ili mpango huo wa maendeleo ya Taifa ufanikiwe, lazima viongozi waongeze kasi ya uwajibikaji na utawala bora.

Naye mwanafunzi wa darasa la 7 shule ya Msingi Mwere A , Seaba Mbega , ameomba vifaa vya TEHAMA Mashuleni vipelekwe ili kurahisisha wanafunzi kujifunza kwa vitendo somo hilo kuanzia shule za msingi.

Pia mwanafunzi Elizabeth Jackson kutoka shule ya Msingi Mwere A, amesomba huduma za afya ziboreshwe kwani bado kuna changamoto kwenye sekta hiyo hususani kwa wamama wajawazito na madirisha ya wazee.

Aidha Mwenyekiti wa chama cha watu wenye Uhalbino Mkoa wa Morogoro(TAS) Hassan Mikazi amesema Dira ya 2050 izingatie watu wenye ulemavu hasa katika Nyanja zote za kielimu,kiuchumi kiafya,  miundombinu na kisiasa.

Tanzania imepitia dira mbili za maendeleo ya Taifa,kwanza ni Dira ya kujipatia Uhuru,msingi wake mkuu ni haki za binadamu,na dira ya pili ilikuwa ni ile ya Azimio la Arusha ambalo lilifafanua falsafa ya ukombozi wa kiuchumi na sasa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeanza kuratibu maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa