• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YAPOKEA WAGENI KUTOKA JIJI LA TANGA

Posted on: November 13th, 2023

Kamati ya Fedha na Uongozi ya Halmashauri ya Jiji la Tanga, ikiongozwa na mwenyekiti wake, ambaye pia ndiye Mstahiki Meya wa Jiji hilo, Mheshimiwa AbdulRahman Omary Shiloow, pamoja na baadhi ya wataalamu kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji hilo, wameitembelea Manispaa ya Morogoro kwa lengo la kujifunza uendeshaji wa kitega uchumi cha stendi ya mabasi ya Msamvu inayokadiriwa kuiingizia Manispaa mapato ya zaidi ya shilingi bilioni mbili kila mwaka.

Akizingumza na wakuu wa vitengo na divisheni za Manispaa ya Morogoro, katika kikao kilichotangulia kabla ya kamati hiyo kuzuru stendi ya Msamvu, Mheshimiwa Shiloow alisema Jiji la Tanga linacho kitega uchumi ambacho kwa sasa ujenzi wake umefikia asilimia 97 hivyo wao kama Kamati ya Fedha na Uongozi wanatamani kuona kitega uchumi hicho kikiimarisha zaidi mapato ya Jiji lao pindi kitakapoanza kufanya kazi.

“Japokuwa kuna msemo usemao kwamba sikio haliwezi kuzidi kichwa, sisi kwa ziara hii, tunategemea tutaweza kwenda kuweka namna bora zaidi ya uendeshaji wa kitega uchumi chetu kwani mwanafunzi hanabudi kufanya vizuri zaidi ya mwalimu wake, na Manispaa ya Morogoro mmekuwa mwalimu mzuri kwetu ndio maana awamu ya kwanza kuna wenzetu walikuja kujifunza na sisi leo tumerudi ili kukazia maarifa” alieleza Mheshimiwa Shiloow.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mheshimiwa Pascal Kihanga, amemshukuru Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga pamoja na timu yake kwa kuichagua Manispaa ya Morogoro kuwa sehemu ya wao kuja kujifunza jinsi ya kuendesha kitega uchumi chao.

“Ninamshukuru Mungu kwamba Manispaa hii ya Morogoro imekuwa chuo cha mafunzo kwani Halmashauri kadhaa zimekuwa zikija kujifunza mambo mbalimbali kutoka hapa na ni imani yangu kwamba nanyi mkishajifunza leo, mtafanya vizuri zaidi” alisema Mheshimiwa Kihanga.

Aidha, wakiwa kwenye kituo cha Mabasi cha Msamvu, wanakamati hao kutoka Jiji la Tanga walipata fursa ya kusikiliza taarifa ya uendeshaji wa kitega uchumi hicho, kutoka kwa meneja wake, wakaona jinsi mifumo ya kielektronki inavyotumika kufuatilia kila kitu kinachotendeka ndani ya kitega uchumi, sambamba na kuona jinsi ukusanyaji wa mapato unavyosimamiwa katika maeneo yote ya kuingilia na ya kutokea.

Stendi ya Mabasi ya Msamvu ni miongoni mwa vitega uchumi vikubwa vya Manispaa ya Morogoro tangu mwaka 2018 ilipokabidhiwa rasmi kwa Manispaa, kutoka mikononi mwa mmliki wa awali, aliyejulikana kama Msamvu Property.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa