• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANYUKI YATWAA UBINGWA MASHAINDANO YA POLISI JAMII KATA YA LUKOBE

Posted on: June 3rd, 2023


TIMU ya soka ya Manyuki Kata ya Lukobe Manispaa ya Morogoro, imefanikiwa kuwa bingwa wa mashindano ya Polisi Jamii Kata ya Lukobe yaliyoandaliwa na Mkuu wa Kituo cha Lukobe Mkaguzi msaidizi wa Polisi Wilaya ya Morogoro ambaye ndiye Mkuu wa Kituo cha Kata ya lukobe kwa kushirikiana na Ofisi ya Kata ya Lukobe.

Akifunga mashindano hayo, mgeni rasmi wa mashindano hayo ambaye ndiye Diwani wa Kata ya Lukobe, Mhe. Selestine Mbilinyi, amesema lengo kuanzishwa Kombe hilo ilikuwa ni kutoa elimu na kuhamasisha jamii kushiriki kwenye ulinzi na usalama wa maisha yao na mali zao.

Mhe. Mbilinyi , amewataka vijana kupenda kushiriki michezo kwani ni ajira, uimarisha afya na ujenga ushirikiano na mshikamano miongoni mwa wananchi.

Timu ya Manyuki imefanikiwa kutwaa ubingwa huo katika mchezo wa fainali wa mashindano hayo, baada ya kuibugiza timu ya Lukobe kwa mikwaju ya penati 4-3 na hivyo kunyakua zawadi ya pesa taslimu Shilingi 200,000/, Kombe na pamoja na mpira mmoja.

Timu ya Lukobe iliyoshika nafasi ya pili ya mashindano hayo imepata zawadi ya fedha taslmu shilingi 100000/= pamoja na mpira mmoja huku mshindi wa tatu Timu ya Tushikamane ikijinyakulia fedha taslmu shilingi 50000/=.

Naye Kamanda wa polisi Kamishina Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Morogoro, ACP . Hassan Maya amempongeza Polisi Kata ya Lukobe, pamoja na uongozi wa kata kwa namna walivyoshirikiana kuratibu na kufanikisha kufanyika mashindano hayo yenye lengo la kuwakutanisha vijana pamoja, kuwapa elimu ya Polisi Jamii ambayo itasaidia kuwaepusha na uhalifu.

ACP Maya, amesema kuwa mwisho wa mashindano haya ndiyo mwanzo wa maandalizi ya mashindano ya mwakani na kuahidi kuboresha na kuongeza zawadi zaidi kwa washindi wa mashindano hayo.

Aidha, ACP Maya, ametumia hadhira iliyofika kushuhudia fainali hiyo kuwataka wananchi wa kata ya Lukobe kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuzuia uhalifu kwa kumpa ushirikiano mkaguzi wa kata aliyepo.

Kwa upande wa Mkuu wa Kituo cha Polisi Kata ya Lukobe, ambaye ndiye muhusika Mkuu wa mashindano hayo, Zuena Mwita, amesema jumla ya timu 8 zilishiriki mashindano hayo ambayo yaliendeshwa kwa makundi hadi kufikia mchezo wa fainali.

Kamanda Mwita, amesema kuwa mashindano hayo yamepata mafanikio kwa kuwafikia watu wengi na kutoa elimu na hamasa iliyokusudiwa lakini imeweza pia kuendeleza michezo kutoka maeneo mbalimbali ya Kata ya Lukobe.

Katika mashindano hayo pia waliibuka wafungaji bora 4, mchezaji bora wa mashindano, kipa bora pamoja na timu bora ambapo kwa kila nafasi zawadi ziliweza kutolewa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa