• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MAPATO YA NDANI BILIONI 1.2 MANISPAA YA MOROGORO YANATUMIKA KUJENGA KITUO CHA AFYA KATA YA TUNGI.

Posted on: August 23rd, 2022

HALMASHAURI ya Manispaa ya Morogoro kwa mara ya kwanza tangu ilipoanzishwa inatekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa Kituo cha kisasa cha Afya Tungi kitakachogharimu kiasi cha Sh bilioni 1.2 , fedha zinazotokana na mapato yake ya ndani.

Kituo hicho cha afya kitakachokuwa na huduma zote muhimu za afya kitahudumia watu takribani 16,793 wanaoishi Kata ya Tungi na nyingine za jirani katika Manispaa ya Morogoro .

Mkurugenzi wa Manispaa Ndg. Ally Machela amesema hayo wakati akizingumza na waandishi wa habari waliotembelea kujionea shughuli za ujenzi wa kituo hicho eneo la kata ya Tungi.

Machela alisema kituo hicho kinajengwa kwa kufuata maelekezo ya Wizara ya Afya na kina majengo 10 ya kutolea huduma mbalimbali kwa wananchi na kwa hatua ya kwanza ujenzi wake umetumia Sh milioni 350 ,fedha zinazotokana na makusanyo ya mapato ya ndani.

“ Kwa sasa tupo katika hatua ya upauaji na tayari tumelipa fedha Sh milioni 83 za ununuaji wa bati na bati hizo wametuahidi wiki ijayo kiwanda kitaleta hizo bati “ amesema Machela

Alisema mradi huo wa ujenzi katika kata ya Tungi umekuwa ni ukombozi mkubwa kwa wananchi wake na wengine wa kata za jirani kupata huduma za afya eneo la karibu .

“ Malengo ya Manispaa yalikuwa ni kujenga kituo cha afya ambacho kimetimia na kwa ujumla tumekidhi vigezo vyote vya majengo yote yanayotakiwa kwa ajili ya mradi wa afya” alisema Machela.

Mkurugenzi wa Manispaa  alisema uamuzi huo ni kwa ajili ya kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha ya kwamba huduma za afya zinafanyika katika kiwango ambacho ni timilifu kwa upatikanaji wa huduma zote muhimu kwa asilimia 100.

“ Ujenzi huu unafanyika kwa fedha za mapato ya ndani ,na Manispaa imeamua kwa makusudi kuhakikisha ya kwamba tuna kuwa na mradi mkubwa unaotokana na mapato ya ndani tuna miradi mingi ya mapato ya ndani lakini huu ni mahususi kwa ajili ya kituo cha afya na mahususi katika sekta ya afya “ alisema Machela

Machela alisema majengo hayo yatawekewa njia maalumu za kupita wagonjwa na watoaji wa huduma katika Kituo hicho .

Machela pia alisema kwa mwaka wa fedha 2022/2023 , Halmashauri imetenga fedha za kumalizia Zahanati nne zilizopo kata ya Kingo , Kauzeni, Mkundi na Mazimbu na ndani ya miaka miwili , Manispaa itakuwa na zahanati zaidi ya 10 zilizokamilika na zinazotoa huduma.

Naye Mganga mkuu wa Manispaa  Charles Mkombachepa alisema kituo hicho cha afya cha kisasa kina majengo hayo 10 ya kutolea huduma ambayo ni jengo la wagonjwa wa nje (OPD), jengo la akina mama wajawazito, jengo la maabara ,jengo la upasuaji akina mama wajawazito, jengo la akina mama wajawazito wanaojifungua na wenye shida mbalimbali za uzazi .

Mganga mkuu wa Manispaa  pia alisema kituo hicho cha afya kina nyumba moja ya mtumishi , jengo la kufulia nguo pamoja na jengo la kuhifadhia maiti .

Nao wakazi wa Kata hiyo akiwemo Leticia Lukanima ameipongeza Manispaa kwa kujenga kwanza Zahanati katika eneo hilo inayowasidia kupata huduma za afya wakiwa karibu tofauti na miaka ya nyuma wakizifuata umbali wa kilometa tano kwenye kata nyingine ya Kichangani kabla ya kuanza mradi huo mkubwa wa kituo cha afya .

“ Tunampongeza Rais wetu kwa kutusogezea huduma hapa Tungi , tunapata huduma nzuri kutoka kwa wauguzi na madaktari na tunaangalia majengo mengine yanayojengwa ya kituo cha afya kikikamilika kitaboresha huduma zaidi na kutuondolea kufuata vipimo vya afya vituo vya mbali “ alisema Leticia

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa