• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MEYA KIHANGA AASA KUHUSU KIPINDUPINDU NA KUWAFARIJI WALIOKUMBQA NA MAFURIKO MOROGORO

Posted on: January 24th, 2024


Mstahiki Meya  wa Manispaa ya  Morogoro, mheshimiwa Pascal Kihanga, ametoa wito kwa waheshimiwa madiwani kuendelea kuwafariji wananchi wa baadhi ya Kata za Manispaa, zilizoathiriwa na mafuriko yaliyotokana na mavua nyingi zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Kihanga ameyasema hayo alipokuwa kwenye Kikao cha Kawaida cha Baraza la Waheshimiwa Madiwani cha Uwasilishaji wa Taarifa za Kata, kiolichofanyika jana, tarehe 23.01.2024, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Manispaa ya Morogoro, ambapo pia amewataka waheshimiwa madiwani pamoja na watendaji wa Kata na Mitaa kuhakikisha wanaendelea kuwaelimisha wananchi kuhusu ugonjwa wa kipindupindu ambao kwa sasa upo katika baadhi ya mikoa nchini.

“Kipindupindu kimeshaingia kwenye mikoa mingine hivyo natoa rai kwenu waheshimiwa madiwani wenzangu tuendelee kuwapa wananchi wetu elimu ya kujikinga na ugonjwa huu, alisisitiza mheshimiwa Kihanga.

Kwa upande mwingine, katika kikao hicho waheshimiwa madiwani wa Kata za Kilakala, Bigwa na Kichangani waliwasilisha taarifa za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Kata zao kwa kipindi cha Robo ya Pili ya Oktoba- Disemba, ambapo Diwani wa Viti Maalum Kata ya  Kilakala, mheshimiwa Mwanaidi Ebrahim Ngulungu emesema kwenye Kata yake Serikali imefanikisha ujenzi wa vyumba nane vya madarasa, mabweni manne na matundu 13 ya vyoo kwenye shule ya Sekondari Kilakala, pamoja na kuanza kwa upanuzi  wa Zahanati ya Kata hiyo, huku wananchi wakiwa wamechangia jumla ya shilingi mia sita themanini elfu (680,000) kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Kata yao.

Kisha Diwani wa Kata ya Kichangani, mheshimiwa Gilbert Barnabas Mtafani akasema, katika Robo hiyo ya Oktoba- Desemba, ndani ya Kata yake, Serikali imefanikisha ujenzi wa jengo la utawala kwenye shule ya Sekondari Kola Hill, na Diwani wa Kata ya Bigwa, mheshimiwa Melichior Peter Mwamnyanyi akasema kwenye Kata yake Manispaa, kupitia fedha za mapato yake ya ndani, imefanikisha ujenzi wa matundu sita ya vyoo kwenye shule ya msingi Mungi huku wananchi wakiwa wanaendelea kuchangia ujenzi wa matundu ishirini ya vyoo kwenye shule ya msingi Misongeni.

Aidha Diwani wa Kata ya Kichangani, mheshimiwa Mtafani ameomba kuimarishwa kwa hali ya ulinzi na usalama ndani ya Kata yake, Diwani wa Kata ya Bigwa, mheshimiwa Mwamnyanyi akaomba miundombinu ya barabara iimarishwe,na Diwani wa Viti Maalum, Kata ya Kilakala mheshimiwa Ngulungu, akasema changamoto inayokabili Kata yake ni uchakavu wa miundombinu na wananchi kutokamilisha miradi wanayoianzisha.

“Mvua zinazoendelea kunyesha zimeharibu miundombinu ya barabara hasa maeneo ya Area 6 na, Njiapanda ya Jordan. Zimeondoa sehemu iliyojengwa mto Kilakala, pia nyakati za jioni maeneo ya Kola A na B, hivi sasa kumekuwa na tabia ya ukwapuaji” alibainisha Diwani wa Kata ya Kichangani, mheshimiwa Mtafani.

MWISHO


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa