• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MEYA MANISPAA AKAGUA MADARASA YA UVIKO-19, ATOA WITO KWA WAZAZI NA WANAFUNZI

Posted on: January 20th, 2022

MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Morogoro na Diwani wa Kata ya Mazimbu , Mhe. Pascal Kihanga, amewataka wazazi wa Wanafunzi Manispaa ya Morogoro kuhakikisha wanafunzi waliofaulu kuingia kidato cha kwanza wote wanawasili shuleni ili kuweza kupata elimu na kutimiza ndoto zao baada ya Serikali kuwatengenezea mazingira rafiki ya kusoma.

Kauli hiyo ameitoa, Januari 20/2022 wakati wa ukaguzi wa Madarasa mapya katika Shule ya Sekondari Kihonda, ambayo madarasa hayo ni miradi ya elimu iliyojengwa kutokana na fedha ambazo Serikali imezipata kutoka Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) kwa ajili ya kupambana na athari za UVIKO-19 na kuzielekeza kuimarisha huduma za jamii.

Akizungumza mara baada ya ziara hiyo, Mhe. Kihanga, amesema kuwa hakuna mzazi anayeruhusiwa kukaa na mtoto bila kupelekwa shule labda kama ana changamoto za kiafya zilizothibitishwa na wataalamu wa afya.

Sambamba na hilo Mhe.KIhanga, amempongeza namna ambavyo Mkuu wa Wilaya ya Morogoro ,Viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM, Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Baraza la Madiwani, Wakuu wa Idara na Vitengo, Watendaji wote, na wananchi kwa kushirikiana bega kwa bega hatimaye kupelekea madarasa yote 86 kukamilika kwa wakati Pamoja na kuwepo changamoto za miundombinu zilizopelekea baadhi ya sehemu kuendesha shughuli za ujenzi kwa kususua.

"Nampongeza sana Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwa kutupatia fedha hizi, tumenufaika kwani tumeweza kujenga madarasa na kuwawekea mazingira mazuri wanafunzi ya elimu kwenye shule zetu , naamini mazingira haya yatapunguza msongamano madarasani lakini kuongeza viwango vya ufaulu , rai yangu wanafunzi wasome kwa bidii na kulinda miundombinu" Amesema Mhe. Kihanga.

Manispaa ya Morogoro ni miongoni mwa Halmashauri zilizopata fedha za Ujenzi wa Madarasa ambapo wamepokea kiasi cha Shilingi Bilioni 1 na Milioni 720 kwa kukamilisha ujenzi wa Vyumba vya Madarasa 86.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa