• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MEYA MANISPAA MOROGORO AWATAKA MADIWANI KUZINGATIA MAADILI KATIKA UTENDAJI WAO

Posted on: December 15th, 2020

MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Morogoro , Mhe. Pascal Kihanga, amewataka Madiwani wa Manispaa ya Morogoro kuzingatia maadili ya kazi katika utendaji wao ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi.

Kauli hiyo ameitoa leo Desemba 15/2020 wakati akizindua mafunzo ya Maadili kwa Madiwani wa Manispaa hiyo ,yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Msamvu Kituo cha Mabasi.

Akizungumza na Madiwani , amesema semina hiyo ya mafunzo ya maadili ni somo muhimu kwa maisha ya kawaida na katika utendaji wao wa kazi katika kuwaongoza wananchi na kutoa huduma.

Amesema kiongozi asiyezingatia maadili kazini hata katika utendaji wake unakuwa na shida kutokana na kukosa misingi ya uadilifu ambayo ndiyo nguzo kuu ya utendaji kazi.

Mhe. Kihanga ,amesema miongoni mwa vitendo ambavyo vinasababisha kukosekana kwa uadilifu wa kazi ni pamoja na kupokea na kutoa rushwa, ubadilifu wa mali za umma, kuwa na mahusiano wa kimapenzi baina ya wafanyakazi wenyewe, kutumia cheo kwa maslahi binafsi, mgongano wa maslahi, tabia ya ulevi , uasherati na ugomvi kwenye jamii ambapo vitu vyote hapo vinamuondolea sifa kiongozi kimaadili.

“Viongozi lazima tuwe waadilifu, hata Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Magufuli , amekuwa mfano kwa kujaza na kusaini hati ya uadilifu inayosimamiwa na tume ya maadili na viongozi wa Umma na viongozi wote tulioteuliwa tumekula kiapo hicho , kwahiyo tutambue kazi zote tunazo zifanya kwa wananachi wetu ni kwaniaba ya Mhe. Rais kwa kufuata maudhui na maadili kama Rais wetu anavyofanya, niwaombe sana mzingatie maadili lakini matarajio yangu ni kwamba Madiwani wote mtakula kiapo cha maadili leo “ Amesema Mhe. Kihanga.

Amesema kuwa matarajio yake baada ya mafunzo hayo madiwani watakuwa wameweza kupata maarifa ya kimkakati yatakayoweza kuwasaidia kuwaongoza Wananchi wao.

Naye, Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amewaomba Madiwani kuwa wasikivu kwakuwa watoa mafunzo wamekuja kuwafundisha na wanajua nini ambacho wanatakiwa kuwasaidia .

Katika hatua nyingine, Lukuba, amewapongeza madiwani pamoja na Wakufunzi kwa kukubali kufanya semina hiyo huku akiwakumbusha na kuwaomba Madiwani kuendelea kutoa huduma kwa kuzingatia Maadili , kanuni na taratibu za nchi kwa maslahi mapana ya Taifa.

“Nawashukuru sana wageni wetu kutoka tume ya Secretarieti ya maadili Kanda ya Mashariki Morogoro na Tanga , pamoja na Wakufunzi kutoka Chuo cha Hombolo Dodoma kwa kutukubalia kuendesha mafunzo yetu, naamini baada ya mafunzo haya tunategemea Madiwani wetu wataendesha kazi zao kwa kuzingatia maadili katika utoaji huduma kwa wananchi wao”” Amesema Lukuba.

Naye, Diwani wa Kata ya Kilakala, Marco Kanga, amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kwa hatua mbalimbali za kuhakikisha Baraza la Madiwani linakuwa chachu ya maendeleo.

‘’Ni mafunzo mazuri upande wetu, hii sio mara ya kwanza lakini tunakumbushwa zaidi ili kuendana na mabadiliko ya uongozi uliopo madarakani ambapo uanataka kila kiongozi awe na maadili kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wake” Amesena Mhe. Kanga.

Kwa upande wa Afisa kutoka Secretarieti ya Maadili Kanda ya Mashariki Morogoro na Tanga , Zaynab Kissoky , amesema lengo la kutoa mafunzo hayo ni kutokana na changamoto mbalimbali katika upande wa maadili kwa Watumishi wa Umma kitu kinachopunguza ufanisi katika kufikia malengo ya kazi.

Mbali na mafunzo amesema Madiwani watajaza na kusaini hati ya uadilifu kama ilivyo kwa viongozi wengine wa Umma.

Miongoni mwa maada zilizowasilishwa ni pamoja na Historia ya Uhalali wa Serikali za Mitaa, Sheria za Uendeshaji wa Mamlaka ya MSM, Muundo, Madaraka na Majukumu ya MSM,Maadili, pamoja na Taratibu za Uendeshaji wa Vikao na MSM.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa