• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MGANGA MKUU WA MANISPAA AZUNGUMZA NA WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII MASUALA YA MAMA NA MTOTO, MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA NA LISHE

Posted on: March 22nd, 2024

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa Morogoro Dkt. Maneno Fucus amefanya kikao na wahudumu wa afya ngazi ya jamii, wa kata za Manispaa na kuwataka wapeleke elimu ya afya ya mama na mtoto, magojwa yasiyo ambukiza, masuala ya lishe, ukatili wa kijinsia, ukatili dhidi ya watoto, dharula za kiafya, na usafi wa mazingira kwenye maeneo wanayoishi.

Katika kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Manispaa ya Morogoro leo tarehe 22.03.2024 Dkt. Focus amewataka wahudumu hao kufahamu mifumo ya kutoa taarifa pindi dharula mbalimbali za kiafya zinapotokea kwenye maeneo yao waweze kuwasiliana na wasimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya wa Manispaa.  

“Eneo la mama na mtoto bado tuko nyuma sana. Kwa mwaka 2023 tu tumekuwa na vifo takriban 200 vya watoto wachanga na akina mama 42 na bado tunapata wajawazito wanaofika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya wakiwa wamechelewa sana yani bado dakika chache wajifungue kutokana na sababu mbambali ikiwemo imani potofu kwamba ukiwahi kwenda hospitali utafanyiwa upasuaji.

“Nendeni mkawahimize wanawake wawe wanaanza kliniki chini ya wiki 12 za ujauzito maana kuna vipimo muhimu hufanywa wakati huo ikiwemo kipimo cha wingi wa damu ili kama kuna upungufu uanze kushughulikiwa mapema ifikapo muda wa kujifungua mjamzito asipate shida, pia kupitia vipimo vya awali tunaweza kuzuia wajawazito wasipate watoto wenye changamoto za kimaumbile kwa sababu watapewa madini muhimu yanayosaidia uumbikaji wa mtoto” alifafanua Dkt. Focus.

Kwa upande wa elimu ya lishe, Dkt. Focus amewataka wahudumu wa afya ngazi ya jamii kuhakikisha wanaendelea kutoa elimu hiyo kwa wajawazito, wazazi, walezi wa watoto kwani vichanga wengi waliofariki mwaka jana 2023 vifo vyao vilisababishwa na uzito mdogo unaoweza kuchangiwa na lishe duni kwa mama wakati wa ujauzito.

Eneo lingine ambalo Dkt. Focus amelizungumzia ni la ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto, ambapo amewataka wahudumu wa afya ngazi ya jamii waibue matukio ya ukatili kwenye maeneo yao na kuyatolea taarifa kwa maafisa ustawi wa Manispaa waliopo kwenye kata na makao makuu kwa ujumla. Amesema kufanya hivyo kutasaidia kuondoa ukatili huu ambao unaweza kumwachia madhara ya kudumu ya kisaikolojia mtoto aliyefanyiwa vitendo hivyo.

Aidha, Dkt. Focus amewataka wahudumu wa afya ngazi ya jamii kutoa elimu ya afya kuhusu magonjwa yasiyoambukiza kama vile shiniko la damu na saratani mbalimbali ili wananchi wawahi kwenda kupima na kupewa matibabu na ushauri wa kiafya pindi wanapokuwa na dalili za magonjwa hayo, na kwa walioanza matibabu wahimizwe kuendelea kuhudhuria kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kwa ajili ya kupata huduma zaidi.

Kwa upande wake Mratibu wa Huduma za Mama na Mtoto wa Manispaa ya Morogoro ndugu Vijan Shaban amesema, jambo kubwa analowataka wahudumu wa afya ngazi ya jamii kulifanya kwenye maeneo yao ni kuifundisha jamii dalili za hatari za wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua ili kuzuia vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi.

Pia amewataka wahudumu hao kupeleka kwa jamii elimu ya uzazi wa mpango kwani inaonesha vifo vingine vya mama na mtoto vinasababishwa na akina mama kubeba ujauzito mfululizo bila kupumzika.

Nao wahudumu wa afya ngazi ya jamii wamemshukuru sana Mganga Mkuu wa Manispaa pamoja na timu yake kwa kufanya nao vikao mara kwa mara kisha wakaahidi kwenda kutekeleza yale yote ambayo wameagizwa kuyafanya.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa