Mhe .Rais Dk John Magufuli amehahidi kumwagiza Waziri wa Maji na Umwagiliaji kufika mkoani Morogoro kushughulikia na kutatua shida kubwa ya uhaba wa maji kwa ajili ya matumizi ya wananchi na viwanda ikiwa ni pamoja na kutolewa fedha ziizotolewa na Jumuiya ya Ulaya kwa ajili ya upanuzi wa Bwawa la Mindu.
Rais Magufuli alisema hayo wakati wakiwahutubia mamia ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na wa halmashauri ya wilaya ya Morogoro baada ya kuzindua Kiwanda kipya cha sigara cha Mansoor Ltd cha kutengeneza sigara aina ya Marlboro kilichopo eneo la Mkambalani , wilaya ya Morogoro.
Kabla ya kuhutubia , Rais alimpa fursa Mbunge wa Jimbo la Morogoro mjini, Abdulaziz Abood kusema kidogo akiwawakilisha wabunge wa mkoa wa Morogoro.
Akizungumza mbele ya Rais , Mbunge huyo alisema , licha ya wawekezaji kujitokeza kuwekeza katika viwanda,mkoa wa Morogoro hasa Manispaa ya Morogoro ,lakini kumekuwa na shida ya upatikanaji wa maji kwa wananchi na viwanda .
Abood alisema ,Manispaa ilikuwa ikitekelezwa mradi wa maji wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP) na waziri mwenye dhamana ya Maji na Umwagiliaji alisema kuwa zimetengwa Euro milioni 70 na ilipaswa kutangaza zabuni lakini zaidi ya mwaka mmoja jambo hilo halijafanyika.
Mbunge huyo alimwomba Rais aweze kusaidia jambo hilo ili mradi huo uweze kutelezwa kwa ajili ya kuwezesha upatikanaji wa maji ya kutosha safi na salama ya kuhudumia uwekezaji wa viwanda na kwa matumizi ya wananchi.
Rais alisema , amepokea ombi la Mbunge huyo la kuomba maji kwa wananchi wa mkoa wa Morogoro kuwa jambo hilo amelibeba kwa nguvu zote na kuagiza wizara husika juu ya fedha Euro milioni 70 za utekelezaji wa mradi wa maji zitolewe ili zifanye kazi inayokusudiwa.
Alisema , Serikali italibeba jambo hilo ili kulifanyia kazi kwa ajili ya kuwezesha upatikanaji wa maji mkoani Morogoro, mkoa wenye mito mingi lakini unakosa maji kwaajili ya matumizi ya viwanda na wananachi.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro
Anuani: 166 morogoro
Simu: 0232614727
Simu: 0734-039300
Baruapepe : info@morogoromc.go.tz
Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa