• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKURUGENZI MANISPAA AWAONYA WAKANDARASI WAZAWA KUACHA TABIA YA KUJIKONGOJA WANAPOAMINIWA NA KUPEWA MIRADI MIKUBWA.

Posted on: May 13th, 2020

MKURUGENZI wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amewaonya Wakandarasi wazawa kuacha tabia ya kujikongoja wanapoaminiwa na kupewa miradi mikubwa katika Manispaa yake , huku akionyesha kutoridhishwa na kasi ndogo ya Ujenzi wa Kitega Uchumi DDC unaoendelea kwa sasa.


Hayo ameyasema leo Mei 13,2020 wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo inayoendelea Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza na Waandishi wa habari, Lukuba ,amesema kuwa ni lazima wahakikishe miradi wanayokabidhiwa na Serikali inakamilika kwa wakati.


Kufuatia kudolora kwa ujenzi wa DDC, Lukuba, amemuagiza Mhandisi wa Manispaa ya Morogoro, Eng.Juma Gwisu, kuhakikisha muda waliopewa wa ujenzi wa mradi huo wakamilishe na hana mpango wa kuongeza muda mwengine.

“”Hawa ndugu zetu tuliwaamini sana , walianza kwa kasi kubwa licha ya kuwaongezea muda lakini bado sijaridhishwa na kiwango cha Ujenzi wa mradi huu,nimeongea na msimamizi wa mradi huu analeta sababu zisizo na msingi wakati tayari tumelipa fedha, najua waliomba waongezewe muda lakini hapana ni bora ningekuta kuna maendeleo ninge fikiria lakini bado hali ipo vile vile “ Amesema Lukuba.



Aidha, amemtaka msimamizi wa ujenzi huo kuongeza nguvu kazi ili ujenzi uendelee kwa kasi kwani muda uliobakia ni mdogo sana.

Lukuba, amesema kuwa, kwa mujibu wa mkataba ujenzi huo wenye thamani ya Shilingi Milioni 635, ulitakiwa kukabidhiwa mwezi Mei 20,2020 lakini mpaka sasa haujakamilika licha ya kuongezewa muda wa mwezi 1 ambapo sasa watatakiwa kuukabidhi mwezi Mei 25, 2020.



Katika hatua nyengine, Lukuba, ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa Stendi mpya ya Daladala Mafiga huku akimtaka Mkandarasi wa mradi huo kuongeza kasi zaidi na kuukabidhi mradi huo kwa wakati kama walivyokubaliana.



“Nimefurahishwa na kasi ya ujenzi huu wa Stendi ya daladala , tumekubaliana mpaka ikifika Mei 25,2020 wawe wametukabidhi mradi huu , niwaombe waongeze kasi ili tukabidhi mradi huu kwa wananchi ambao wamekuwa wakiusubiria kwa hamu sana, endeleeni kufanya kazi usiku na mchana natumaini hiyo asilimia 4% iliyobakia mtaimaliza kwa wakati”” Amesema Lukuba.





Hata hivyo, amewaeleza wananchi wa Manispaa ya Morogoro kuwa Serikali yao ya awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ipo makini na itahakikisha ina kamilisha kwa asilimia 100 miradi yote ya maendeleo ili kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.



Mwisho, amewataka wakandarasi wote wanaosimamia miradi katika Manispaa ya Morogoro, wafanye kazi kulingana na walivyosainiana mikataba kwani fedha ambazo wanatumia ifikapo mwezi Juni 30, 2020 zitarudishwa hivyo kuna athari ya wenye miradi na waliochukua tenda kuzikosa fedha hizo.



Kwa upande wa Mhandisi wa Manispaa ya Morogoro, Eng. Juma Gwisu, amesema atahakikisha fedha za miradi hazirudi Serikalini , hivyo atakula nao sahani moja wakandarasi ili fedha hizo ziendelee kutumika katika miradi hiyo.



Gwisu , amesema ujenzi wa mradi wa Stendi ya Daladala Mafiga mpaka sasa umefikia asilimia 96% huku miradi mingine ikiendelea vizuri na ujenzi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa