• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKURUGENZI MANISPAA MORO, AWATAKA WAKUU WA IDARA KUWEKA MALENGO HALISI ILI KUFIKIA KIWANGO CHA JUU KATIKA UTENDAJI KAZI.

Posted on: November 20th, 2019

MKURUGENZI wa Manipsaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, leo Novemba 20, 2019, amefungua mafunzo kwa Wakuu wa Idara juu  ya uzingatiaji wa kanuni, sheria na taratibu za Utumishi wa Umma.

Akizungumza katika ufunguzi wa kikao hicho , amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo Wakuu wa idara pamoja na kutoa huduma bora na kuzingatia miiko ya kazi na kuweka malengo halisi ya kazi ili kufikia kiwango cha juu katika utendaji wa kazi .

Amesema kuwa mafunzo hayo yameendeshwa na wawezeshaji kutoka Chuo kikuu Mzumbe , hivyo amewaomba watumishi kuzingatia mafunzo hayo  muhimu kwani yanawajengea uwezo watumishi kimaadili katika kazi  zao za  kila siku.

"Tumewaandalia mafunzo haya ikiwa ni sehemu ya wajibu wangu kama mwajiri wenu wa kuwajengea uwezo ili hatimaye muweze kuongeza ufanisi wa kazi kila mmoja katika eneo lake la kazi, nyinyi ni watu muhimu sana kwenye taasisi yoyote, nawaomba mjiamini vya kutosha ,muwe familia moja." Amesema  Sheilla.

Aidha, amekipongeza Chuo Kikuu cha Mzumbe kwa kujitoa kwao katika ushirikiano wa mafunzo hayo pamoja na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, akisema matarajio yake ni kwamba baada ya mafunzo hayo watumishi watazingatia  vizuri miiko ya kazi na kutoa huduma bora kwa Wananchi pamoja na kutunza siri za ofisi.

Naye Afisa Utumishi wa Manispaa ya Morogoro Waziri Kombo, amesema mafunzo hayo yamehudhuriwa na jumla ya Wakuu wa idara 19 na wasaidizi 30, huku akitarajia kila mkuu wa idara na wasaidizi wake mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo watatoa huduma bora kwa Wananchi wao.

Pia amesema  kuwa,mafunzo hayo yamewalenga wao kwani ndio wanaosimamia idara  hivyo amewataka wabadilike na kuendana na kasi ya Mhe.Rais Dkt John Magufuli ya kuchapa kazi kwa bidii pamoja na kufuata misingi ya utawala bora.

" Niwaombe watumishi wenzangu, ufanyaji kazi umebadilika, Rais wetu anahitaji matokeo chanya kwa maendeleo ya Taifa,  hivyo lazima tubadilike ili kuendana na kasi yake pamoja na kuweka utaratibu mzuri wa muda wa kusikiliza Wananchi na muda wa kufanya kazi zako"" Amesema Kombo

Katika hatua nyengine, Afisa Mifugo na Uvuvi Manispaa ya Morogoro, Ndg. Mohamed Chamzhim,  amemshukuru Mkurugenzi wa Manispaa kwa  kuandaa mafunzo hayo kwani yatawajengea uwezo mkubwa wa kuwatumikia wananchi na kutoa huduma bora ikiwamo kuzingatia miiko kazini na kuweka malengo ya kiutendaji.

 Kwa upande wa Mratibu wa Kuzuia na kudhibiti maambukizi ya Ukimwi, Manispaa ya Morogoro, Upendo Elias,   amesema wao wameyapokea mafunzo hayo na kuahidi kutoa ushirikiano kwa wakufunzi wa mafunzo kwani yataleta tija kubwa katika utoaji wa huduma bora.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa