• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKURUGENZI MANISPAA MOROGORO AMUAGIZA AFISA MAZINGIRA NA USAFISHAJI KUSIMAMIA UENDESHAJI WA DAMPO LA TAKATAKA

Posted on: January 13th, 2020

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amemtaka Afisa Mazingira na usafishaji Manispaa ya Morogoro  kuhakikisha anaweka mikakati ya kueleweka katika uendeshaji wa dampo la takataka lililopo kata ya Mafisa.

 Akizungumza na Waandishi wa Habari , amesema hajaridhishwa na Uongozi wa Dampo hilo kutokana na uharibifu unaoendelea kufanywa na Viongozi hususani katika suala zima la uchimbaji wa Vifusi vya mchanga na kuvipeleka sehemu isiyojulikana.

Aidha, amesema katika kikao cha kusikiliza na kutatua kero za Wananchi mnamo Januari 8, 2020 kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi, St. Monica Kihonda, kuliibuka kero za kwamba kuna zoezi la uchimbaji wa  Vifusi unaoendelea katika Dampo hilo.

"Nipo hapa Dampo, ni  kweli nimejionea mwenyewe uharibifu uliopo kiasi kwamba taka taka zinashindwa kufikishwa sehemu husika kwa jinsi dampo lilivyoharibika, viongozi  wa dampo hili  wanahusika moja kwa moja kwani badala ya kutoa maelekezo ya umwagaji mzuri wa taka wao wanaruhusu taka kumwagwa njiani, nimemwagiza bwana  afya hili swala alishughulikie na wale wote waliohusika nitawachukulia hatua " Amesema Sheilla.

Amesema kilichomsikitisha zaidi ni kwamba mtambo wa gari wanalozolea kifusi ni wa  Manispaa na mafuta wanatoa Manispaa lakini hakuna hata pesa au chanzo chochote cha mapato  wanachokipata kutoka katika dampo hilo jambo ambalo hawezi kulivumilia huku akimtaka bwana afya kuwa mkali la sivyo wote watawajibishwa kwa mujibu wa sheria na matumizi mabaya ya mali za Umma.

Katika hatua nyengine amesema kama bwana afya hata kuwa mkali kwa hilo na kushindwa kuchukua hatua atatafuta mwenyewe walinzi watakao kuwa wanalinda na kuweka Uongozi utakaokuwa na maslahi kwa Manispaa na kuchangia mapato kwa ajili ya maendeleo.

Naye Afisa Mazingira na usafishaji  Manispaa ya Morogoro, Samwel Subi, amesema wamepokea ushauri wa Mkurugenzi wa kusimamisha shughuli zote za uchimbaji Vifusi.

Pia amesema kuwa, kwa sasa wanakabiliwa na changamoto za kuharibikiwa na mitambo miwili ya magari ya taka ambapo baada ya Mkurugenzi kutoa maelekezo wameshaanza kuyatengeneza na wana amini baada ya ya matengenezo hayo kero za taka zitakuwa zimetaturiwa na kuwaondolea wananchi kero ya moshi, harufu mbaya pamoja na kuzaliana kwa nzi.

Amesema kwa Sasa Manispaa ipo katika mchakato wa kutengeneza Dampo la Kisasa baada ya kupata eneo jipya Mkundi na kwasasa wapo katika mpango wa kulipa fidia kwani Dampo  hilo kwa sasa lipo karibu na makazi  ya watu hivyo kusababisha kero kwa wananchi.

Kuhusu uchimbaji wa Vifusi katika dampo hilo,amesema wameshatoa maelekezo kwa Meneja wa Dampo kwamba yeyote atakayeonekana anachimba kuchukuliwa hatua za kisheria.

"Tumeshaongea na wananchi, Uongozi wa Mtaa pamoja na Mhe. Diwani wa kata hii ya Mafisa kwamba kama wataona mtu yeyote anachimba vifusi watoe taarifa kwa ajili ya utekelezaji wa kumchukulia hatua za kisheria,  na kama ni mtumishi hatua za kinidhamu zitachukuliwa" Amesema Subi

Amesema kuwa Vifusi vilivyopo vitumike katika kufukia takataka katika dampo hilo, ili ziweze kuoza kwa urahisi na kuzuia nzi wasiendelee kuzaliana.

Kwa upande wa Mkazi wa eneo hilo, Yusuph Abdallah amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kwa hatua aliyochukua ya kupiga marufuku uchimbaji wa vifusi pamoja na kufuatilia maendeleo ya dampo hilo.

Amesema Uongozi wa Dampo hauwatendei haki kabisa kwani taka zimezagaa hovyo kiasi kwamba zinapelekea magonjwa ya milipuko.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa