• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKURUGENZI MANISPAA YA MOROGORO AKABIDHI TV NA KING'AMUZI KITENGO CHA USTAWI WA JAMII

Posted on: April 9th, 2021

Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro Sheilla Lukuba , amekabidhi TV Flat Screen pamoja na Kingámuzi cha AZAM kwa Kitengo cha Ustawi wa Jamii Manispaa ya Morogoro.

Tukio hilo la makabidhianao hayo limefanywa na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Dr. Ikaji Rashidi, ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Manispaa ya Morogoro leo Aprili 9/2021 kwenye Jengo Jipya la Ofisi ya Ustawi linalotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni.

Vifaa hivyo vyenye thamani ya Shilingi laki 750,000/= amevitoa ikiwa ni jitihada zake za kufanya maboresho katika Kitengo cha Ustawi ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na kutoa huduma bora.

Ikaji, amesema lengo la kutoa Tv hiyo ni kuwafanya wateja wanaofika Ofisini kufuata huduma waweze kutazama vipindi mbalimbali vyenye kutoa elimu pamoja na kupata taarifa mbalimbali zinazoendelea na kuona maendeleo yanayofanywa na Serikali.

Amesema kuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, licha ya msaada huo lakini amekuwa mstari wa mbele sana katika kusaidia Idara ya Afya na Kitengo cha Ustawi kwani mara kwa mara amekuwa akijitoa kwa hali na mali kusaidia makao ya kulelea Watoto yatima pamoja na makao ya wazee kwa kuwapatia huduma mbalimbali ikiwamo huduma za vyakula pindi wanapohitaji huduma hizo amekuwa haachi nyuma.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Ustawi wa Manispaa ya Morogoro, Hamisa Kagambo, amemshukuru Mkurugenzi kwa msaada alioutoa kwani itawasaidia wateja wanaofuata hudma kuweza kupunguza msongo wa mawazo kipindi anapotoka nyumbani akiwa amekorofishwa au kuwa na jambo ambalo limekuwa na presha ya hali ya juu.

Kagambo, amemuomba Mkurugenzi wa manispaa ya Morogoro aendelee na moyo wa kuwasaidia kwani mbali na alichokitoa bado Kitengo hicho cha Ustawi kinakabiliwa na changamoto mbalimbali za huduma huku akimtakia kazi njema katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku.

Naye Mmiliki wa kituo cha kulelea watoto wadogo (day care) Rainball kilichopo Kata ya Kihonda Maghorofani, Abdallah Sakibu, amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, kwa kuwa mstari wambele kusaidia Ustawi wa Jamii kwa kutoa vifaa hivyo lakini kubwa zaidi kwa kuwajengea Ustawi wa Jamii jengo la Ofisi kwani sasa wanaamini Jengo hilo litakuwa suluhisho la kuweka usiri mkubwa baina ya wateja na wafanyakazi.

Amesema kuwa, awali wateja wamekuwa wakipata shida sana wanapofika Ofisi za Ustawi kwani wamekuwa wakipishana na watumishi wengi jambo ambalo linamfanya mteja kushindwa kuelezea tatizo lake kwa uwazi zaidi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa