• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKURUGENZI WA MANISPAA AWAONYA MGAMBO KUTONYANYASA WAFANYABIASHARA

Posted on: November 21st, 2023

Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, ndugu Ally Machela amelaani vikali kitendo cha baadhi ya mgambo kuwapiga machinga, badala yake amewataka mgambo wajue kwamba kazi yao ni kusimamia usalama wa raia na sio kuwapiga ama kuwanyanyasa kwa namna iwayo yote ile na kwamba mgambo ye yote atakayebainika kwenda kinyume na maelekezo ya Manispaa katika kutekeleza majukumu yake, Manispaa itamchukulia hatua kali za kisheria.

Mkurugenzi Machela ameyasema hayo mapema asubuhi leo tarehe 21.11.2023 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wa kituo cha redio na televisheni Abood, waliomtembelea ofisini kwake ili aueleze umma wa Morogoro na Tanzania kwa ujumla mafanikio ambayo Serikali ya Awamu ya Sita, kupitia Manispaa ya Morogoro imeweza kuyafikia ndani kipindi cha miaka miwili tangu mwaka 2021 hadi sasa.

 “Hivi karibuni tulipokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya baadhi ya mgambo kumpiga mwanamke mmoja mjasiriamali na kumsababishia majeraha yaliyompelekea kulazwa hospitalini. Sisi kama Manispaa tunalaani kabisa kitendo hicho, na mgambo wote waliohusika kwenye tukio hilo tayari tumekwisha kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria na sisi kama Manispaa hatuwahitaji tena kwa ajili ya kufanya nao kazi” alieleza Machela.

Mkurugenzi Machela amewataka wafanyabiashara wote waendelee kuheshimu kufanya biashara kwenye maeneo waliyopangiwa na Manispaa huku wakifuata sheria zilizowekwa na Manispaa kuhusu ufanyaji wa biashara.

Vilevile, Mkurugenzi Machela amewataka machinga waliopo eneo la Faya wapuuze uvumi kwamba Manispaa itawafurusha kwenye eneo hilo mara baada ya ujenzi wa soko jipya la machinga kukamilika. Amesema kwamba Manispaa haina mpango wa kufanya hivyo na pia Manispaa haiwezi kuhamisha wafanyabiashara kwenye maeneo waliyopo sasa bila kushauriana na kushirikiana na viongozi wa Wilaya na Mkoa.

“Kwenye soko jipya la machinga linalojengwa kule Faya, tutawapeleka machinga waliopo mtaani, na zoezi la kuwatambua machinga hao tayari linaendelea kutekelezwa. Kwa machinga waliopo kwenye maeneo ya muda mfupi, wataendelea kuwepo na kufanya shughuli zao kwenye maeneo hayo. Kadiri tutakapokuwa tukijenga maeneo ya kudumu tutaendelea kuwahamisha” alifafanua Machela.

Kwa upande mwingine, Mkurugenzi Machela ameueleza umma mafanikio ambayo Manispaa ya Morogoro imeweza kuyafikia katika sekta za elimu, afya, ardhi, biashara, Barabara, kilimo, mifugo na uvuvi kwa kipindi cha miaka miwili tangu mwaka 2021 hadi sasa, kupitia fedha kutoka Serikali Kuu na Makusanyo ya Mapato ya Ndani ya Manispaa.

“Katika sekta ya afya Manispaa tumefanikiwa kujenga Zahanati 12, vituo vya afya viwili, na hospitali moja ya Wilaya iliyopo kwenye Kata ya Mkundi. Sekta ya Elimu Msingi tumejenga shule mpya nne kwenye Kata za Mafisa, Mindu, Kihonda Maghorofani na Kilakala. Sekta ya Elimu Sekondari tumejenga vyumba vya madarasa 167 kwenye shule mbalimbali zilizokuwa na upungufu wa madarasa, tumejenga shule mpya nane kwenye Kata za Mbuyuni, Mazimbu, Tungi, Mkundi, Lukobe, Mindu, Mzinga na Boma, na shule sita kati ya hizo mpaka sasa zinao wanafunzi wa kidato cha kwanza na pili huku mbili zilizosalia ziko katika hatua ya ukamilishaji.

Pia, katika sekta ya ardhi tumefanikiwa kutatua migogoro 3,727 ya ‘double location’ kwa kupitia mradi wa Manispaa wa upangaji na upimaji wa ardhi kwenye eneo la Kiegea, hivyo kwa sasa Manispaa haina mgogoro wo wote wa ‘double location’ ya ardhi. Na kwa upande wa kilimo, wakulima zaidi ya elfu nane wananufaika na mbolea za ruzuku kutoka Serikali Kuu, tunaanzisha kilimo cha zao la karafuu na tunajenga machinjio mpya ya kisasa huko kwenye Kata ya Mkundi kwani machinjio tuliyo nayo sasa bado ni ile iliyojengwa miaka ya 1950, ambayo kwa sasa haikidhi mahitaji ya idadi ya wananchi waliopo sasa na inachangia kwa kiasi fulani uchafuzi wa mazingira” Alieleza kwa kina Machela.

Mkurugenzi Machela amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Manispaa kufikisha huduma za maendeleo kwa wananchi wake kupitia fedha nyingi za miradi ambazo Serikali imekuwa ikizileta kwenye Manispaa na kufanikisha utekelezaji wa miradi kwenye sekta za elimu, afya, kilimo na hata ardhi.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa