• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKUU WA WILAYA MOROGORO ARIDHISHWA NA UTENDAJI WA KAMATI YA USHAURI WILAYA

Posted on: November 18th, 2019

MKUU wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo, amefurahishwa na matokeo ya utendaji wa kamati ya Ushauri Wilaya na kuwataka wajumbe waendelee kuhamasisha jamii kwa ajili ya kuchangia masuala mbali mbali ya maendeleo katika Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza na Waandishi wa habari, amesema lengo la Kamati ya ushauri Wilaya ni kuhakikisha Manispaa inasonga mbele, hivyo wajumbe wasichoke na wawe huru kutoa mapendekezo yao kwa kuchangia mambo mbali mbali kwa mustakabadhi wa maendeleo ya Wilaya.

Akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu maendeleo ya sekta ya elimu , amesema wanafunzi waliofaulu darasa la saba mwaka jana 2018, wote walifanikiwa kujiunga na kidato cha kwanza, akisema hayo ni maendeleo ya jitihada za Wajumbe wa Kamati ya ushauri katika kukuza elimu kwa Manispaa ya Morogoro.

Aidha, amesema mwaka huu, Wanafunzi wote wa darasa la saba wamefaulu na wanatakiwa kujiunga kidato cha kwanza  mwaka 2020, lakini  kuna changamoto ya upungufu wa madarasa 35  na mpango uliopo ni  kila shule ya Sekondari kuongeza madarasa mawili.

"Niwaombe Wajumbe wa kikao cha Kamati ya ushauri wilaya, endeleeni kuhamasisha jamii kwa ajili ya kuchangia ili tuweze kupata msaada wa ujenzi wa madarasa, maana wakisema wachukue idadi ya Wanafunzi 45 kwa kila darasa wengi wataachwa na watashindwa kufika kidato cha nne na kutotimiza ndoto zao" Amesema DC Chonjo.

Kuhusu Vijana wanaoosha magari nje ya Ofisi ya Chama Cha Mapinduzi CCM, amesema alishatoa maagizo lakini nashangaa mpaka leo Vijana hao wapo na wanaendelea kuosha magari katika eneo hilo ambalo sio maalumu kwa kazi hiyo na agizo lake limepuuzwa.

" Afisa Mazingira hapa umenikosea, inaonesha umepuuza agizo la kamati, kazi nakupa wewe na wewe unakazi ya kusema agizo ni la DC basi kama huiwezi hiyo kazi niifanye mwenyewe kuwaweka mgambo na kazi haifanyiki ni kupuuza agizo langu, narudia tena hao vijana watoke na muwatafutie maeneo maalumu ya kuoshea magari, maeneo yetu mengi yana water table (mzunguko wa maji).Aliongeza DC Chonjo

Aidha, amesema suala la mazingira kwa Manispaa ya Morogoro bado ni kizungumkuti, hivyo amemtaka Mstahiki Meya wa Manispaa na Mkurugenzi kupitia upya mikataba ya vikundi kazi vya usafishaji mji.

"Mhe. Mstahiki Meya nikuombe kaeni na baraza lako , suala la usafi Manispaa yetu bado ni tatizo, vikundi hivi havina uwezo wa kufanya kazi na watu wanalipa pesa zao taka hazizolewi kwa wakati kaeni mpitie mikataba yao upya na muone jinsi gani mnaweza kutatua changamoto hiyo kwani  ni aibu Manispaa za wenzetu zinaongoza kwa usafi yetu hata kumi bora haipo " Amesema DC Chonjo.

Pia amemtaka Afisa Mazingira pamoja na MORUWASA kulifanyia ukarabati wa kuliziba shimo lililo pembezoni mwa Soko kuu  kwani shimo hilo limekuwa kubwa  kutokana na usugu wa kumwaga maji taka kwa wafanyabiashara wa mama lishe waliopo pembezoni mwa bara bara na kuleta athari kwa watumiaji wa bara bara hiyo.

Mbali na mazingira, DC Chonjo, amemuagiza Afisa biashara kuwaondoa haraka watu wanaodaiwa kufanya kazi mkabala na Soko kuu la kisasa kwani eneo hilo sio rasmi la wao kufanya biashara zao.

Akichangia suala la uharibifu wa bara bara , Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro, Ndg. Fikiri Hassan Juma, amesema kuna tabia imezuka ya malori makubwa kufanya maegesho ya magari  pembezoni mwa barabara katika pande zote mbili jambo ambalo linahatarisha maisha ya watumiaji wa bara bara na kuharibu barabara kutokana na uzito wa malori hayo.

Akijibu hoja ya Maegesho, Meneja wa TARURA Mhandis James Mnene amekili kuwepo kwa changamoto hizo, lakini amesema wana kikosi kazi kinachotembea hadi usiku kwa ajili ya kuangalia maegesho ya malori makubwa barabarani.

Aidha, Mhandisi Mnene amesema kuwa tayari wale wahusika  waliokamatwa tayari wamefikishwa mahakamani na kesi zipo kwa mwanasheria wao , huku akisema kuwa ushauri wa DC ameupokea na wataongeza jitihada zaidi ya kuyafanyia kazi mapendekezo ya  Wajumbe wa kamati ya Ushauri Wilaya.

Kuhusu Ujenzi wa Darasa la Shule ya Msingi Tubuyu, Afisa Mtendaji wa Kata ya Tubuyu, Justine Masaba, amesema darasa limeshatengenezwa na wapo katika hatua ya kutengeneza choo cha shule lakini Mkuu wa Wilaya amesema wale wote walisababisha hasara ya kujenga darasa jengine watachukuliwa hatua za kisheria.

Naye aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Morogoro aliyestaafu , Mhe. Steven Mashishanga, ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa kusimamia  vyema mapendekezo ya kamati ya ushauri lakini amesema ni vyema katika vikao vijavyo vya kamati kila idara ikaonesha takwimu halisi katika taarifa zake zikiwamo changamoto , idadi ya upungufu wa watumishi ili kamati iweze kutoa ushauri.

Katika kuhitimisha hilo, DC Chonjo, amewataka Wananchi watakapoona kuna kero ambazo zinaleta madhara watoe taarifa kwake haraka ili kuzuia madhara yasiendelee kutokea.

Askofu Yohana, ameipongeza Manispaa ya Morogoro kutokana na jitihada za kutokomeza vibaka na kuweka miundombinu mizuri ya barabara na kuwataka waendelee na kasi zaidi ili Manispaa iwe na maendeleo makubwa.

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Morogoro, Ndg. Fikiri Juma, ameshauri kuwepo na usafiri kwa watumishi kwani kukosekana kwa usafiri kunawafanya watumishi kutofika maeneo ya wananchi kwa aharaka na kutoa huduma.

Aidha, amesema huduma ya zima moto kwenye nyumba za ibada ni changamoto, hivyo ameshauri MORUWASA na Zima Moto watenge maeneo ya kuchukulia maji inapotokea majanga ya moto.

Amesema bara bara ni nzuri lakini hakuna mazingira ya kuridhisha , pamoja na vyoo pembezoni mwa bara bara mfano uwanja wa mashuja hauna choo wananchi wanajisaidia hovyo.

Pia , amesema Manispaa ya Morogoro haina kituo cha afya cha ramani ya TAMISEMI, hivyo ameshauri kujengwe angalau vituo 3 vya kuanzia ili huduma iweze kumfikia mwananchi kwa karibu.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amewataka Watendaji na wakuu wa idara wanapoandika taarifa zao kwenye vitabu viendane na uhalisia wa taarifa zilizopo kwenye miradi. Aidha amewataka Watendaji kila mmoja kutimiza wajibu wake na kuangalia thamani ya miradi iliyopo ili iweze kusaidia maendeleo ya vizazi vijavyo.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoroo, Mhe. Pascal Kihanga, amewataka Wajumbe wa kamati ya ushauri kuzungumzia changamoto na kutoa ushauri kwa uhuru ili yatokanayo yaweze kufanyiwa kazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa