• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MORO WAWEKA MKAKATI WA KUONGEZA VIFAA VYA UCHUNGUZI NA UANGALIZI KUPUNGUZA MAGONJWA YA MOYO

Posted on: September 30th, 2018

Hospitali ya rufaa mkoa wa Morogoro imeweka mpango mkakati wa kupunguza idadi ya wagonjwa wanaopoteza maisha kwa kuongeza vifaa vya uchunguzi na uangalizi kwa kila mgonjwa anayeshambuliwa na magonjwa ya mishipa pamoja na moyo.

Mganga Mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro, Dk Rita Lyamuya alisema hayo katika maadhimisho ya siku ya magonjwa ya moyo Duniani Septemba 29, mwaka huu kwa mkoa wa Morogoro.

Katika maadhimisho hayo ya kimkoa , mgeni rasmi alikuwa ni mkuu wa mkoa , Dk Kebwe Stephen Kebwe ambaye aliwakilishwa na mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo.

Mganga Mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa alisema ,magonjwa ya moyo sasa yamekuwa ni tishio kwa wananchi na nimoja ya magonjwa yanayoongoza kuua watu wengi barani Afrika , Ulaya na Amerika kwa ujumla kutokana na kiharusi , shinikizo la damu na mshituko wa mishipa ya moyo.

Dk Lyamuya alisema , hospitali ya rufaa inatoa huduma za kliniki kila wiki ambayo hutolewa na madaktari bingwa na idadi ya wagonjwa ambao wanaohudhuria inafikia 2,500 hadi 3,000 kwa mwaka .

Pia alisema, wagonjwa wa ndani kwa maana wanaolazwa wanafikia 1,000 hadi 1,500 kwa mwaka na wanaolazwa kutokana na shinikizo la damu ni 876 kwa mwaka.

Alisema , bado zipo changamoto mbalimbali kwa wananchi ikiwa na uelewa mdogo wa magonjwa hayo juu ya kijikinga , upungufu wa wataalamu na vifaa hivyo kusababisha ongezeko la rufaa kwa wagonjwa na gharama zake.

Dk Lyamuya alishauri kuwepo kwa ongezeko la bajeti ya dawa ya maradhi ya moyo ,kuongeza wataalamu katika fani ya mishipa ikiwa na kutolewa elimu kwa wananchi jinsi ya kuepuka vichocheo vinavyoweza kusababisha maradhi ya moyo .

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Morogoro, Chonjo katika hotuba yake aliwashauri wananchi wa mkoa  kutambua kuwa , magonjwa ya moyo si ya kuambukizwa na yanajitokeza kutokana na mbalimbali yakiwemo ulaji usio sahihi, mazingira tunayoshi na kutofanya mazoezi ya mwili.

Hivyo aliwaomba wananchi kufanya mazoezi mara kwa mara, kuepuka ulevi na kurekebisha aina ya ulaji kulingana na malekezo ya wataalamu na kuwa na tabia ya kuchunguza afya zetu mara kwa mara .

Chonjo pia aliuagiza uongozi wa hospitali ya rufaa kuwa , pamoja na siku ya maadhimisho hayo yaliyoanza Septemba 28 na kufikia tamati Septemba 29, mwaka huu suala la upimaji wa afya kwa wananchi uendelee hadi kufikia Oktoba 6, mwaka huu.

“ Leo ni maadhimisho ya siku hii ya magonjwa ya moyo duniani , lakini shughuli hii iendelee eneo la viwanja vya hospitali hiyo hadi kufikia Oktoba 6, mwaka huu ili kutoa fursa kwa wananchi wengi wa manispaa kupata huduma hii bure “ alisema Chonjo.

Nao baadhi ya wananchi waliojitokeza kuchunguza afya zao siku ya kilele hicho mjini Morogoro kwa nyakati tofauti walipongeza Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) , na Serikali ya Tanzania kwa kuanzisha siku hiyo maalumu kwa kutoa elimu na upimaji.

Walisema , baadhi yao wameweza kuzitumia siku hizo kufika kupima na kujitambua iwapo wanazo dalili na magonjwa ya moyo au shinikizo la damu na kupewa ushauri wa kitaalamu wa namna ya kujikinga nayo na kuchukua tahadhari ya mfumo wa ulaji wa vyakula na kufanya mazoezi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa