• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MORUWASA YAKABIDHIWA MRADI WA MAJI MTAA WA KASANGA

Posted on: August 28th, 2017

Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro imekabidhi shughuli za uendeshaji na matengenezo ya mradi wa Maji wa Kasanga kwa Mamlaka ya Maji na usafi wa mazingira (MORUWASA).

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa Bw Ignas Sanga ameeleza kuwa mradi huo ni miongoni mwa miradi iliyotekelezwa kupitia Awamu ya kwanza ya Program ya maendeleo ya Sekta ya Maji(WSDP1).Lengo la mradi ni kutoa huduma ya maji safi ,salama na ya kutosha kwa wakazi wapatao 6,890 wa mtaa wa Kasanga na Mzaga ifikapo 2025.Aidha alieleza kuwa gharama za mradi ni shilingi 443,187,738.00 ikiwa ni fedha kutoka Serikali kuu kupitia Mfuko wa pamoja wa Maendeleo ya Sekta ya Maji.

Kaimu Mkurugenzi Bw Sanga ameeleza mradi wa Maji wa mtaa wa Kasanga ulifikiwa mara baada ya wananchi wa mtaa huo kuuibua mnamo mwaka 2007 ambapo uliingizwa kwenye Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji kwa ajili ya kufanyiwa upembuzi yakinifu na ujenzi wa mradi ulianza tarehe 10/12/2014 na kukamilika tarehe 16/04/2016.

Akipokea mradi huo Mkurugenzi wa MORUWASA Bw Nicholaus Angumbwike ameeleza kuwa kukabidhi mradi huu kwenye Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Morogoro ni utekelezaji wa matakwa ya kisheria ambapo kifungu Na.13(1) cha sheria ya Maji na Usafi wa Mazingira Na.12 ya mwaka 2009 kinaelekeza kuwa Mamlaka za Maji ndio zenye dhamana ya kisheria ya kutoa huduma ya maji na usafi wa mazingira katika maeneo yao ya kiutawala.

Aidha Bw Angumbwike. alieleza kuwa wananchi kupitia vikao vilivyofanyika kuanzia ngazi ya mtaa mpaka ngazi ya Halmashauri kwa hiari yao waliikubalia na Halmashauri kukabidhi mradi huo kwaajili ya shughuli zote za uendeshaji na matengenezo hivyo Halmashauri haitahusika tena na uendeshaji na matengenezo ya mradi huo.

Pia ameeleza faida za mradi huo kwa wakazi wa mtaa wa Kasanga kuwa ni pamoja na kuboresha kipato cha wananchi kwa kutumia mda mfupi kupata maji safi na salama,kupunguza magonjwa yatokanayo na matumizi ya maji yasiyo safi na salama,na kujenga mazingira mazuri ya wanafunzi wa shule ya msingi ya Kasanga na shule ya Sekondari ya Bondwa ya kuwa na mda mwingi wa kujisomea badala ya kutafuta maji.

Naye Mkurugenzi huyo ameupongezaa uongozi wa Manispaa ya Morogoro kwa kuusimamia toka kuibuliwa kwa mradi huo hadi hatua ya ujenzi na hatimaye kukamilika.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa