• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AITAKA JAMII KUONGOZA KUTOKOMEZA UKIMWI

Posted on: November 27th, 2023

Naibu  Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, mheshimiwa Ummy Nderiananga ametoa rai kwa jamii kutafakari nafasi waliyonayo katika kupinga kwa nguvu zote masuala yote na tabia hatarishi zinazochangia maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (VVU), ikiwemo unyanyapaa, ukatili wa kijinsia, mila zinazochangia maambukizi, ngono katika umri mdogo, na kuporomoka kwa maadili.

Mheshimiwa Nderiananga ametoa rai hiyo leo tarehe 27.11.2023, katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Nashera Morogoro, alipokuwa akifungua rasmi Kongamano la Kitaifa la Kisayansi, lenye lengo la kutathmini mafanikio, changamoto, na mwelekeo wa Taifa katika kutekeleza lengo la kutokomeza UKIMWI nchini ifikapo mwaka 2030, pamoja na kutoa taarifa za kisayansi zitakazoboresha afua za UKIMWI nchini.

“Kama Taifa tunahitaji kuihamasisha jamii kuwa mstari wa mbele kuweza kutoa mchango wake katika kufikia azma ya kutokomeza UKIMWI kwa kuzuia maambukizi mapya hasa kwa kundi la vijana hasa wasichana ambao kwa mujibu wa takwimu, ndio wenye kiwango kikubwa cha maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (VVU) hapa nchini” alieleza mheshimiwa Nderiananga.

Vilevile, mheshimiwa Nderiananga amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mheshimiwa Daktari Samia Suhulu Hassan kwa utayari na uimara wake wa kuonesha kwamba Serikali inao uwezo wa kutenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha inaendeleza mapambano dhidi ya UKIMWI hapa nchini, kwani katika mwaka huu wa fedha Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya mapambano hayo na kazi inaendelea.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, mheshimiwa Adam Malima amesema Sayansi imekuwa na mchango mkubwa sana katika kuwasaidia watanzania na Taifa kwa ujumla kuwa na uelewa kuhusu ugonjwa wa UKIMWI kiasi kwamba hivi sasa hata wanandoa wenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi wanaweza kupata watoto wasio na maambukizi.

“Kwenye miaka ya 1990 ilikuwa ukipata UKIMWI ni hukumu ya kifo, na unyanyapaa ulikuwa mkubwa sana ndani ya jamii hivyo watu wengi waliokuwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) walifariki kutokana na kutokuwa na uelewa wa ugonjwa huu pamoja na unyanyapaa, lakini sasa hivi Sayansi imetusaidia sana kuushinda ujinga dhidi ya ugonjwa huu” alisema Malima.

Naye mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na UKIMWI (UNAIDS), ndugu Mohamed Toure ametaja umasikini uliokithiri kuwa ndio kichochezi kikubwa cha maambukizi mapya ya Virusi vya UKIMWI katika nchi za Afrika, ambapo amesema takwimu za mwaka 2022 za hali ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI duniani zinaonesha kwamba nchi za ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara, ikiwemo Tanzania, ndio zenye kiwango kikubwa cha watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (VVU), huku kundi la vijana wa kike wenye umri kati ya miaka 15 hadi 24 likiwa ndilo linaloongoza kwa kuwa na watu wengi wenye maambukizi hayo.

“Kati ya watu 3,600 wanaopata maambukizi mapya ya Virusi vya UKIMWI kila siku duniani, asilimia hamsini ni kutoka kwenye ukanda wa Jangwa la Sahara, na 360 kati yao ni watoto wenye umri chini ya miaka 15 huku 3,200 wakiwa ni watu wenye umri wa miaka 15 na kuendelea na ambao kati yao asilimia 40 ni wanawake, asialimia 30 ni vijana wenye umri wa miaka 15 hadi 24 na asilimia 18 ni wasichana wenye umri kati ya miaka 15 hadi 24” alifafanua ndugu Toure.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa