• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

OFISI YA WAZIRI MKUU YAWAOMBA WADAU KUONGEZA KASI YA KUDHIBITI ONGEZEKO LA MAAMBUKIZI YA VVU

Posted on: October 21st, 2019

Ofisi ya Waziri Mkuu imesema , masuala ya udhibiti wa maabukuzi ya virusi vya ukimwi ni budi yaendelee kupewa kipaumbele kuanzia ngazi ya jamii , wilaya , mkoa , kitaifa ili kuhakikisha kuwa Tanzania inafikia lengo la kimataifa la 90-90-90.

Hivyo, ni kwa maana ya ( asilimia 90 ya wanaoishi na VVU watambue hali zao , asilimia 90 ya WAVIU wawe wameanza dawa za kupunguza makali ya VVU na asilimia 90 ya walianza dawa wapunguze kiwango cha virusi mwilini) ifikapo 2020.

Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri mkuu , Paul Sangawe alisema hayo ( Okt 18, 2019) baada ya kuwasilishwa taarifa ya Uratibu wa Ukimwi ya Manispaa ya Morogoro .

Timu ya ujumbe wa maofisa kutoka Ofisi ya waziri mkuu, Tume ya kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) pamoja na TAMISEMI pia walitembela Konga ya Manispaa ya Morogoro .

Sangawe alisema , ni muhimu kwa wakati huu kuunganisha wadau wa kuchangia shughuli za udhibiti wa Ukimwi ili kuweza kupewa kipaumbele kuanzia ngazi ya wilaya , mkoa na taifa .

Hata hivyo aliipongeza Halmashauri ya Manispaa  ya Morogoro kwa kutenga bajeti na kuzitoa fedha hizo na kutumika , lakini ni vyema kujua jinsi zilivyotumika na kama zimeweza kuwasaidia walengwa .

“ Lazima kuwe na muunganiko wa kutengwa bajeti, utoaji wa fedha na matumizi yake iwapo yanawanufaisha walengwa “ alisema Sangawe.

Mbali na hayo alitaka mpango wa miaka mitano wa lishe unaotekelezwa katika Ofisi ya Waziri mkuu kuwa shughuli zake ziendelee kwa kushirikiana na wadau wengine licha ya mradi wa Sauti Yetu ufadhili wake kumalizika tangu Septemba mwaka huu (2019).

Naye Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathimini kutoka TACAIDS , Dk Jerome Kamwela akiwa katika Konga ya Manispaa ya Morogoro eneo la Kata ya Mbuyuni ,alisisitiza umuhimu wa wadau mbalimbali na jamii kuongeza nguvu juu ya kudhibiti ongezeko la maambukizi ya VVU.

Awali, Mwenyekiti wa Konga Manispaa ya Morogoro , Kellen Mpesa katika taarifa yake alisema , moja na jukumu lake ni kuhamasisha na kuunda vikundi vya WAVIU , kuhamasisha upimaji wa VVU kwa jamii , kuwaibua na kusaidia wagonjwa ambao wamepotea kwenye huduma bila taarifa zozote na wanaougua majumbani .

Pamoja na hayo alisema , Konga ya Manispaa imeunda vikunzi zaidi ya 20 na 11 na kati ya hivyo nane vinajishughulisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi vikiwa na wanachama 172 kati hao 145 wanawake na 27 wanaume.

Katika hatua nyingine , Asasi ya kiraia inayojishughulisha na watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI pamoja na watu wanaoishi katika mazingira magumu HACOCA iliyopo Manispaa ya Morogoro imeweza kuwafikia watu 15,058 kati ya 16,716 waliolengwa kufikiwa katika kipindi cha mwaka 2016/2019

Mratibu wa Mradi wa kizazi kipya katika Asasi hiyo, Veronica Anonsisye alisema hayo kwa wajumbe kutoka Ofisi ya Waziri mkuu , Tacaid na Tamisemi waliofanya ziara ya tathimini ya baadhi ya miradi ya UKIMWI mkoani Morogoro .

 Kwa mujibu wa Mratibu wa Mradi wa Kizazi Kipya wa Asasi hiyo kuwa , watu hao wamejengewa uwezo katika masuala ya kiuchumi, lishe bora , elimu na dawa za kufubaza maambukizi ya virusi vya UKIMWI

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa