• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RAS NA MEYA WAGAWA MICHE ZAIDI YA 4000 YA MIKARAFUU KWA WANANCHI WA MILIMANI

Posted on: April 29th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ally Mussa ameshirikiana na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro mheshimiwa Pascal Kihanga kugawa miche zaidi ya elfu nne (4,000) ya mikarafuu kwa viongozi wawakilishi wa wananchi wa Kata za Bigwa, Kilakala, Magadu, Luhungo, Boma na Mlimani.

Akizungumza na wenyeviti wa mitaa, wajumbe, wakulima na baadhi ya waheshimiwa madiwani kabla ya ugawaji wa miche hiyo kwenye uwanja wa Ofisi za Kilimo za Manispaa ya Morogoro, Dkt. Mussa amemshukuru Mstahiki Meya pamoja na menejimenti ya Manispaa kwa kuridhia kununua miche ya karafuu na kuigawa bure kwa wananchi wa Kata za milimani ikiwa ni jitihada za makusudi za Manispaa kuhakikisha uhifadhi wa mazingira katika milima ya Uluguru.

Dkt. Mussa amewataka wananchi wote watakao gawiwa miche hiyo wahakikishe wanaipanda na kuitunza kwa sababu mikarafuu haitasaidia kutunza mazingira peke yake bali itakapo zaa itakuwa ikivunwa na kuuzwa na hivyo itakuza pato la wananchi.

“Jamani hii miche ni mali. Hakikisheni mnaipanda kwa wingi na kuitunza ili ikue. Leo miche zaidi ya elfu nne itakabidhiwa kwenu lakini tunayo ahadi ya miche elfu 30 kutoka kwa watu wa bonde, na yote hiyo ni kwa ajili yenu.

“Tunafanya yote haya kuhakikisha tunaunga mkono jitihada za rais Samia za kuinua pato la wananchi. Manispaa yetu imedhamiria kuinua kiwango cha maisha ya wananchi wake ndio maana inaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kununua miche ya mikarafuu na kuigawa bure kwa wananchi” alieleza Dkt. Mussa.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro mheshimiwa Pascal Kihanga amesema, lengo namba moja la Manispaa kukubali kujaza miche ya mikarafuu kwenye milima ya Uluguru ni kutunza mazingira ya milimani.

“Nataka watu wa milimani mjue kwamba kama Manispaa tumeshaamua kwamba hamtahama huko milimani kupisha uharibifu wa mazingira, badala yake tunataka mpande miti ya mikarafuu maana itasaidia sana kuyahifadhi mazingira na kuwaweka ninyi salama.

Nao viongozi wawakilishi wa wananchi wa Kata za milimani miongoni mwao wakiwemo waheshimiwa madiwani, wamemshukuru sana Katibu Tawala wa Mkoa Dkt. Mussa Ally Mussa kwa kuleta njozi hii njema ndani ya Manispaa, na wameahidi kuwasimamia wananchi wote watakaopewa miche, wanaipande na kuitunza.

Leo ni awamu ya pili ya mgao wa miche ya mikarafuu kwa wananchi, awamu ya kwanza jumla ya miche elfu mbili (2,000) itolewa.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa