• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RC MALIMA AWATAKA WANAWAKE KUPAZA SAUTI WANAPOKUMBANA NA UKATILI WA WA KIJINSIA

Posted on: March 11th, 2024


Vitendo vya ukatili wa kijinsia vinaendelea kuongezeka siku kwa siku ndani ya mkoa wa Morogoro lakini Kamati ya Usalama ya mkoa imeshaanza kuandaa mkakati kabambe wa kuvidhibiti na ikibidi kuvitokomeza kabisa.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, mheshimiwa Adam Kighoma Malima alipokuwa akizungumza na wananchi wa mkoa huo, kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo hufanyika kila mwaka tarehe 08 mwezi wa tatu.

Mheshimiwa Malima amewataka wanawake, ambao ndio kundi linaloonekana kuathiriwa zaidi na vitendo hivyo kuliko wanaume, kutokaa kimya pindi wanapofanyiwa vitendo vya ukatili badala yake wapeleke taarifa kwenye Dawati la Jinsia la Polisi, ama kwenye Ofisi za Ustawi wa Jamii ili kuweza kupata msaada wa kisheria.

Pia, ameitaka Mahakama pamoja na Taasisi zinazoshughulika na masuala ya haki za binadamu, kuongeza kasi katika kutoa elimu ya aina za ukatili wa kijinsia na haki za akina mama waliomo katika mifumo ya ukatili wa kijinsia.

Mbali na ukatili wa kijinsia, mheshimiwa Malima amewapongeza wanawake kwa kuwa warejeshaji wazuri wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmshauri mbalimbali nchini ukilinganisha na kundi la vijana na watu wenye ulemavu ambao pia hunufaika na mikopo hiyo.

Aidha, mheshimiwa Malima amempongeza Rais Samia kwa kuwa mfano wa kuigwa na wanawake wote ndani na nje ya Tanzania, jambo linalopelekea wanawake wakiwemo wa mkoa wa Morogoro kuendelea kutoa michango yao kwa ajili ya maendeleo ya mkoa na nchi kwa ujumla.  

Kwa upande wao wanawake wa mkoa wa Morogoro ambao sauti zao ziliwasilishwa kupitia Risala iliyosomwa mbele za Mkuu wa Mkoa, wamemshukuru Rais Samia kwa kujenga shule za bweni maalum kwa ajili ya watoto wa kike kwenye mikoa mbalimbali nchini na mkoa wa Morogoro ukiwa miongoni mwayo kwani jambo hili linaonesha jinsi gani Serikali inapamabana kuwekeza kwa mwanamke ili kuharakisha maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii kwa ujumla.

Mwisho, wameiomba Serikali iongeze jitihada katika kupambana na ukatili wa kijinsia katika maeneo yote nchini kwa kutunga sheria zitakazo wabana wale wanaojihusisha na vitendo hivyo.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa