• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RC MORO AWAAGIZA MA DED KUSIMAMIA KUTOZALISHWA KWA HOJA ZA UKAGUZI.

Posted on: May 15th, 2019

Mkuu  wa Mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen Kebwe amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri za wilaya za mkoa  wa Morogoro kuwachukulia hatua za kinidhamu na kisheria watendaji wa mitaa, vijiji, kata na wakuu wa idara ambao wamesababisha kuzalisha hoja za ukaguzi ama kushindwa kuwashilisha fedha za makusanyo ya ushuru wa mapato benki.

Dk Kebwe alitoa agizo hilo katika hotuba yake juzi kwenye kikao cha Baraza Maalumu la kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa Fedha wa 2017/2018 kwa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Pia amesikitishwa kuona Halmashauri ya Kilombero na Ulanga kupata hati zenye mashaka na hivyo kupoteza sifa ya kupata fedha toka serikali kuu za miradi ya maendeleo ya kimkakati kwa muda wa miaka mitatu mfululizo.

“ Mkoa una Halmashauri tisa za wilaya , lakini mbili zimetuangusha , ni Ulanga na Kilombero na hapa hatua kali zitachukuliwa kwa waliohusika kuzifikisha hapo zilipo” alisema mkuu wa mkoa na kusisitiza.

“ Sasa ninaagiza kwa wakurugenzi wote wa Halmashauri za mkoa huu na wenyeviti wa halmashauri chukueni hatua kali za kinidhamu na za kisheria kwa haraka wote waliosababisha kuzalisha hoja za ukaguzi wakiwemo na wasiowasilisha benki fedha za makusanyo ya ushuru” alisema Dk Kebwe.

Alisema, mara nyingi hoja za ukaguzi hazijalishiwi na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali , bali na baadhi ya watendaji wa halmashauri husika wasio waaminifu kuanzia wa mitaa, vijiji pamoja na wakuu wa idara kwa kushindwa kutimiza majukumu waliyopewa kuyasimamia.

Hata hivyo alizitaka Halmashauri za wilaya hizo pamoja na Manispaa ya Morogoro kuzifanyia kazi kwa kujibu hoja zote za ukaguzi kwa wakati na pia kusimamia utekelezaji wa maagizo ya kamati za Bunge .

Naye Mkaguzi mkuu wa Nje wa mkoa a Morogoro, Mwabwanga Peter akisoma taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa Fedha wa 2017/2018 alisema ,katika halmashauri saba nchini zilizopata hati zenye mashaka, mbili ni za mkoa wa Morogoro ambazo ni Ulanga na Kilombero.

Hata hivyo aliipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kupata hati inayoridhisha (hati safi ) kwa miaka saba mfululizo na hivyo kuitaka itekeleze maagizo yote kamati ya Bunge ili hoja zilizojitokeza ziweze kufutwa kwa mujibu wa sheria.

Mbali na hayo aliitaka Manispaa kuanza kujipanga kuweka mifumo mizuri na madhubuti ya usimamizi wa miradi ya kimkakati ikiwemo stendi ya mabasi ya Msamvu na Soko kuu baada ya kukamilishwa ujenzi wake ili iwe endelevu kuleta faida kwa wananchi na kuepuka kuzalisha hoja za ukaguzi kipindi cha uendeshaji .

Kwa upande wake , Meya wa Manispaa , Pascal Kihanga pamoja na kumshukuru Rais Dk John Magufuli kwa kutoa fedha za ujenzi wa soko la kisasa ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 41alisema ,huo ni ukombozi kwa Manispaa ya Morogoro kuekelea kujitegemea kiuchumi.

“ Tukikabishiwa stendi ya mabasi ya Msamvu ambayo Rais aliagiza na pia kukamilika kwa ujenzi wa soko kuu la kisasa pamoja na miradi mingine ya kimkakati itakayojengwa , halmashauri yetu itakuwa na uchumi wenye kuimarika ambao utachangia kukuza shughuli za maendeleo ya wananchi “alisema Kihanga.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa