• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RC MWASSA AAHIDI USHIRIKIANO KUKUZA MICHEZO MKOANI MOROGORO.

Posted on: April 17th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa ameipongeza Taasisi ya Fountain Gates Schools kwa kuonesha nia ya kuwekeza katika michezo Mkoani Morogoro na kuahidi kutoa ushirikiano ili kuhakikisha kuwa nia hiyo inatimia.

Mhe. Mwassa ameyamesema hayo Aprili 12, 2023 wakati akiwapongeza wachezaji na viongozi wa timu ya wanawake ya Fountain Gates ambayo imechukua ubingwa wa kombe la Afrika kwa mashindano ya Shule za Sekondari mwaka 2023 baada ya kukutana na Mkuu huyo wa Mkoa Ofisini kwake.

Mhe. Fatma Mwassa amesema anaipongeza Taasisi ya Fountain Gates kwa wazo la kuweka kituo cha michezo Mkoani Morogoro kwani amebainisha kuwa kufanya hivyo kutaibua na kuendeleza vipaji vya watoto hususani wakike na kukuza soka la wanawake hapa nchini.

 “...kubwa lililo tufurahisha zaidi ni nia ya Fountain Gate ya kuwekeza katika Sports Accademy hapa kwetu Morogoro, tunawakaribisha sana na tupo tayari kushirikiana nanyi....na tutahakikisha ndoto yenu inatimia...” Amesema RC Mwassa.

Sambamba na hilo Mkuu huyo wa Mkoa ameipongeza timu hiyo kwa kutwaa ubingwa wa Mashindano ya shule za Sekondari barani Afrika kwa upande wa wanawake huku wakitoa mchezaji bora wa mashindano hayo, mfungaji bora na kipa Bora hivyo amewapongeza viongozi wa timu hiyo kwa kujitoa kwao, kuiandaa timu hiyo hadi kutwaa ubingwa huo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wakuu wa Shule za Fountain Gates Tanzania Bw. Joseph Mjingo amesema mafanikio wanayoyapata ni kutokana na sera nzuri ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan husuan katika utekelezaji mzuri wa Mtaala wa elimu na michezo kwa kuifanya michezo kuwa sehemu ya vipindi darasani.

Nae, Naodha wa timu hiyo Felista Richard amesema ushindi walioupata ni kutokana na ushirikiano kutoka Serikalini na kujituma kwao uwanjani huku akiiomba Serikali kutoa fursa kwa vijana kuonesha vipaji vyao ili waweze kuyafikia malengo waliojiwekea.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa