• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RITA YASOGEZA UTOAJI WA HUDUMA YA VYETI VYA KUZALIWA NGAZI YA KATA NA VITUO VYA HUDUMA ZA AFYA KWA WATOTO CHINI YA MIAKA 5 .

Posted on: December 4th, 2019

Registration Insolvency & Trusteeship Agency(RITA) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro imesogeza huduma ya utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya miaka mitano ngazi ya kata na vituo vya kutoa huduma za Afya.

Hayo yameelezwa na Mganga Mkuu wa Manispaa ya Morogoro Dr.Ikaji Rashid kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya kusajili na kutoa Vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri wa miaka mitano kwa wasajili wasaidizi.

Katika mafunzo hayo ambayo yamezinduliwa Desemba 4, 2019 katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa ya Morogoro,Dk. Ikaji, amesema vyeti hivyo vinatolewa bila malipo katika ngazi ya kata na vituo vya huduma za Afya kuanzia tarehe 6-17/12/2019, hivyo hatarajii kusikia Mwananchi yeyote atakayefika ngazi za Kata na vituo vya Tiba kutozwa fedha yoyote kwa ajili ya kupata cheti cha kuzaliwa cha mtoto.

Amesema kupitia mpango huo , kila kituo cha uandikishaji kitapewa simu kwa ajili ya kutuma taarifa za watoto watakaosajiliwa na wananchi watapaswa kufika katika vituo hivyo wakiwa na kadi ya kliniki ya mtoto na tangazo la uzazi,.

“Hakikisheni mnazitunza simu hizi na kuzitumia kwa kazi iliyokusudiwa si kwa matumizi mengine, pia huduma hii ni bure kwa yeyote atakayekiuka utaratibu huu, hatua kazi za kisheria zitachukuliwa dhidi yake na huduma hii itatolewa kwenye vituo tiba vinavyotoa huduma za baba, mama na mtoto hivyo haitakuwa na sababu mtoto kutokuwa na cheti cha kuzaliwa” Amesema Dr Ikaji

Dr Ikaji amesema kuwa kuanzishwa kwa mpango huo kutasaidia kuwaletea Wananchi huduma hiyo, huku akitoa rai huduma hiyo isitumike vibaya kama fursa ya kujipatia kipato kwa wale wote ambao Serikali imewapa dhamana ya kutoa huduma hiyo kwa ngazi ya Kata na Vituo vya Tiba.

Aidha, amesema Mafunzo hayo ni muhimu sana ambayo yataleta suluhisho kwa changamoto zilizokuwa zinasababisha watoto wengi kutokuwa na vyeti vya kuzaliwa .

Amesema mojawapo ya changamoto kubwa ilikuwa ni umbali mrefu kutoka makazi ya Wananchi kabla ya kufika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ambayo ilikuwa inahusika na utoaji wa Vyeti vya kuzaliwa.

Katika hatua nyengine, amechukua nafasi ya kutoa shukrani kwa RITA ambao wanasimamia mpango huo huku akiamini kuwa mpango huo ukitekelezwa kwa ufanisi, utaleta matokeo chanya katika utambuzi wa watoto.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa