• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RUKSA WAMACHINGA KUFANYA BIASHARA NDANI YA STENDI YA MSAMVU

Posted on: May 6th, 2018

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuona ni namna gani ya kuwaruhusu wafanyabiashara wadogo (machinga) kuweza kuuza bidhaa zao ndani ya Kituo cha mabasi Msamvu kilichopo Manispaa ya Morogoro.

Rais Magufuli aliyasema hayo Jana wakati akifungua Kituo cha kisasa cha mabasi cha Msamvu kilichopo mjini hapa ambapo mradi wa ujenzi umegharimu kiasi cha shil. Bil.12.055 na kusimamiwa na kampuni ya ujenzi ya Group Six  kwa kushirikiana kwa ubia kati ya LAPF na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Dkt Magufuli alisema kuwa dhamira ya serikali ni kuhakikisha inajenga vituo mbalimbali vya kisasa vya mabasi ili wananchi waweze kuuza bidhaa zao na kuweza kunufaika na vituo hivyo.

Akitolea mfano wafanyabiashara ndogo ndogo Mkoani Morogoro kudai kuzuiwa kufanya shughuli zao za kuuuza bidhaa zao ndani ya Kituo hicho ikiwemo Chakula na Matunda kwa wasafiri alisema kuwa kitendo cha kuwazuia ni kuwanyanyasa wananchi hivyo Manispaa inapaswa kuwawekea mkakati wa kuwapa vitambulisho ili waweze Ku endelea kuuza bidhaa zao bila kubughudhiwa na mtu yoyote.

"Msiwazuie wamachinga kuuza bidhaa zao bali muwawekee mfumo mzuri kwani naamini hata mkiwaambia wachangie hata hela ya usafi watafanya hivyo" Alisema Rais Magufuli.

"Naagiza hivyo kwani lengo la serikali ni kuboresha maisha ya wananchi wake na sio kuwabagua na tunataka kuona Mkoa wa Morogoro unakuwa wa kisasa na wananchi kuweza kunufaika na fursa zilizopo na zinazozunguka mikoa jirani ikiwemo Dodoma na Dar es salaam. Alisema Rais Magufuli.

Naye Mwenyekiti wa Kampuni ya Msamvu Properties Company Eliudi Sanga akisoma taarifa za mradi wa ujenzi wa Kituo cha mabasi Msamvu alisema kuwa wazo la ujenzi wa kituo hicho cha kisasa ulianza mwaka 2008 baada ya kuona Kituo kilichokuwepo kuwa na mapungufu mengi na hakikuwa kinakusanya mapato ya kuridhisha.

Sanga alisema kuwa baada ya majadiliano ya kina mwaka 2009 Mfumo wa LAPF uliweza kutoa saini na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa ajili ya kuanzia ujenzi wa Kituo cha mabasi cha kisasa eneo la Msamvu na kukiendesha kwa mfumo wa Kampuni.

Aidha Alisema kuwa kabla ya Kampuni hiyo kuanzishwa mapato yalikuwa ni wastani wa shil 350,000 kwa siku lakini baada ya Kampuni kuanza kusimamia hivi sasa mapato yameweza kuongezeka na kufikia shil Mil 3 kwa siku.

" Kutokana na ongezeko hilo tunatarajia kukusanya shil Bil.3.11 katika mwaka wa fedha 2017-2018 ikilinganishwa na shilingi Milioni 515. 5 zilizokusanywa mwaka 2013 .Alisema Sanga

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo wa Jimbo la Morogoro mjini (CCM) Abdulaziz Abood aliiweka wazi mbele ya rais Magufuli kuhusu ubadhiribu Mkubwa uliofanyika katika miradi ya mjini Morogoro.

"Mheshimiwa Rais kuna miradi mingi ya maji imefanyiwa ubadhirifu  fedha mfano mradi wa maji wa Kipera uliotumia shil Mil 500,mradi wa Kiegea,Kasanga,Mkorea, ambapo jumla ya Bili.1.56 zimeteketea na hivyo wananchi kukosa Huduma ya Maji safi Na salama" Alisema Abood.

Abood alisema kutokana na changamoto hiyo ya miradi kuonekana fedha zake zimeteketea na kushindwa kumletea tija mwananchi amemuomba Rais Magufuli aingilie kati ambapo sanjari na hayo Rais amemuagiza Waziri wa TAMISEMI Suleiman Jaffo kufanya uchunguzi Juu ya ubadhirifu huo.

Hata hivyo Kituo cha mabasi cha Msamvu ni miongoni mwa kituo Vya kisasa vlivyojengwa nchini ambapo kinatoa Huduma mbalimbalimbali ikiwemo mfumo WA usalama (CCT kamera,mgahawa Mkubwa wa Chakula,sehemu ya kusubiria abiria,mabenki,vibanda Vya biashara ,jengo la utawala nk.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa