• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA HUDUMA BORA KWA WAZEE: DIWANI KATA YA LUHUNGO MANISPAA YA MOROGORO

Posted on: October 21st, 2021

DIWANI wa Kata ya Luhungo, Mhe. Abdallah Chamgulu, amesema Serikali inaendelea kuboresha huduma kwa Wazee hususani Wazee wa Kata ya Luhungo.

Kauli hiyo ameisema Oktoba 21/2021 katika sherehe za uzinduzi wa Baraza la Wazee Kata ya Luhungo pamoja na kuwasimika Viongozi wa Wazee kuanzia ngazi za Mitaa na Kata.

Akizungumza na Wazee waliojitokeza katika uzinduzi huo wa Baraza la kuwasimika Viongozi, Mhe. Chamgulu , amesema kuwa Serikali inatambua kuwa wazee ni hazina katika kuibua na kuchochea shughuli mbalimbali za kimaendeleo kutokana na ushauri mzuri wanaotoa wanaposhirikishwa katika mambo ya kimaendeleo.

"Serikali itaendelea kujiimarisha katika kuboresha upatikanaji wa huduma bora kwa Wazee kwa kuzingatia umuhimu wa kundi hili katika jamii yetu , Manispaa yetu ya Morogoro kwa kuwatambua Wazee wameanza kutatua changamoto ya vitambulisho vya msamaha wa matibabu bure kwa wazee wetu , hii ni hatua kubwa ambayo Manispaa yetu imeifanya na sio mwisho hapa Luhungo kuna Mitaa 7 lakini Mitaa 4 ndio wazee wamepata vitambulisho na hiyo iliyobakia katika zoezi lijalo basi tutaipunguza na kufanya Mitaa yote 7 inafikiwa na huduma hii"Amesema Mhe. Chamgulu.

Aidha, Chamgulu, amesema kwa Mitaa ambayo haijafikiwa na huduma hiyo ya vitambulisho, Ofisi ya Kata imeandaa utaratibu mzuri wa kuwaandikia barua za kuwatambua wazee hao ili na wao waendelee kupatiwa huduma kama wengine huku wakiendelea na wao kupatiwa vitambulisho vyao.

Katika hatua nyingine, Mhe. Chamgulu, amesema Serikali itahakikisha kwamba wanaenda kutatua changamoto za haraka kwa Wazee kupata stahiki zao mapema pindi wanapo staafu kazi ili waweze kujikimu wakiwa nyumbani.

Naye, Mratibu wa Wazee Manispaa ya Morogoro, Rehema Malimi, amesema katika kuona Baraza hilo la Wazee linatimiza majukumu yake vizuri wataandaa semina kwa viongozi wao ili kila mmoja kujua majukumu yake na mipaka yao katika kuwatumikia wazee.

Malimi, amewahimiza wazee kuwa na utaratibu wa kwenda kucheki afya zao mara kwa mara ili kupata huduma stahiki kwa wakati kwani huduma za afya kwa wazee kuanzia miaka 60 ni bure katika vituo vyote vya kutolea huduma.

Kupitia Uzinduzi huo wa Baraza na kuwasimika Viongozi, Bi. Malimi, alitumia fursa hiyo kuwakumbusha wazee hao juu ya UVIKO-19 na kuwataka wazee kuendelea kuchanja, kwani wapo kwenye kundi ambalo ni rahisi kupata maambukizi hayo huku akiwatoa hofu kwamba chanjo hii ni salama kabisa na kuwataka kumuunga mkono Mhe.Rais alieona umuhimu wa kuokoa maisha ya watanzania kwa kupata chanjo hii.

Naye, Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Manispaa ya Morogoro, Mzee Samweli Mpeka, amezitaja baadhi ya changamoto zinazowakabili wazee ikiwa ni pamoja upungufu wa dawa na wataalam wa kuhudumia wazee,umaskini uliokithiri kutokana na kipato duni au kutokuwa na kipato kabisa sambamba na wazee kutokupewa kipaumbele kama makundi mengine kama vile wanawake,vijana na walemavu.

Halmashauri ya manispaa ya Morogoro imeungana na Kata ya Luhungo , katika sherehe za Uzinduzi wa Baraza la Wazee Kata ya Luhungo pamoja na kuwasimika Viongozi wa Mabaraza hayo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa