• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

SERIKALI YA AWAMU YA TANO KUSHUGHULIKIA KERO YA MAJI MANISPAA MORO

Posted on: November 5th, 2018

Mbunge wa Jimbo la Morogoro mjini , Abdulaziz Abood,amewahakikishia wananchi wa Manispaa ya Morogoro kuwa ,serikali ya awamu ya tano imejipanga kumaliza changamoto zote zinazowakabili ikiwemo ya upatikanaji wa huduma bora  ya maji safi na salama .

Mpango huo ukiwa ni pamoja na kujengwa kwa soko la kisasa na kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya kisasa ya wilaya itakayowezesha kupatikana kwa huduma za kisasa cha tiba kwa wananchi.

Abood alisema hayo juzi wakati wa ziara ya kukagua na kuhimiza shughuli za maendeleo katika Kata ya Mwembesongo , Mazimbu na Mji mpya zilizopo Manispaa  ambapo pia alichangia fedha na vifaa vya kumalizia miradi iliyopo katika kata hizo.

Alisema, siku zote kitu ambacho alikuwa akikipigania kwa nguvu zote anapokuwa Bungeni ni kuhusu tatizo la maji katika Manispaa ya Morogoro ambapo sasa Serikali imetambua jambo hilo na kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya kumaliza tatizo la maji.

“ Binafsi nikiwa bungeni nimebatizwa jina la bwana maji, maana kila nikisimama nazungumzia maji, kwakuwa ninajua tatizo kubwa kwa wananchi wangu ndio hilo” alisema Abood na kuongeza kwa kusema .

“ Nashukuru sasa tayari serikali imeshanielewa , na tumepata mradi mkubwa wa maji na tayari mkandarasi ameshasaini kuanza kazi mara moja na muda si mrefu tutaondokana na tatizo hili” alisema Abood.

Kuhusu hospitali ya wilaya alisema, amewasiliana na Waziri wa TAMISEMI  na amehamikishia kuwa zitatolewa fedha kwa ajili ujenzi wa wodi ya kisasa, chumba cha upasuaji na nyumba ya mganga ili iweze kutoa huduma bora kwa wakazi wa kata zilizopo pembezoni mwa Manispaa .

Mbunge huyo alisema , licha ya kuchangia ujenzi wa zahanati kila kata ,amewalipia bima ya afya (CHF iliyoboreshwa ) wazee wote kila kata ili kupata huduma za matibabu katika zahanati na vituo vya afya.

Kuhusu sekta ya elimu alisema , ametoa mifuko 100 ya saruji na nondo kwa kila darasa linalojengwa kila kata ili kumaliza changamoto ya upungufu wa madarasa.

Kwa upande wa Meya wa Manispaa ya Morogoro, Pascal Kihanga ambaye ni Diwani wa kata ya Mazimbu alisema, kupitia Mbunge huyo shughuli za kimaendeleo zimefanyika na kukamilishwa ikiwemo kupata fedha kwa ajili ya ujenzi wa soko la kisasa , kujengwa barabara za kiwango cha lami na kuiwezesha Manispaa kuwa na sifa ya kuelekea kuwa Jiji.

Hivyo alisema , katika kuboresha huduma za usafiri tayari Manispaa inatarajia kujenga stendi ndogo ya kisasa ya mabasi yanayofanya safari ndani ya Manispaa pamoja na eneo la maegesho ya magari makubwa ya mizigo.

Naye Ofisa Mtendaji wa kata ya Mazimbu, Alatutosia Sanga alimshukuru mbunge kwa kutoa Sh milioni sita kwa ajili ya kusaidia uboreshaji wa mazingira mto Ngerengere ambao ulikuwa ukimwaga maji kwenye makazi ya wananchi wa Mazimbu na ujenzi wa zahanati , vyumba vya madarasa ya shule ya msingi Mazimbu A na B.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa