• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

TAASISI YA DR NTUYABALIWE YASISITIZA ELIMU YA KUSOMA VITABU KWA WANAFUNZI SHULENI.SASA YAVUKA NJE YA DAR ES SALAAM

Posted on: March 27th, 2018

Wanafunzi wa shule ya Msingi Uhuru iliyopo Manispaa ya Morogoro wametakiwa kujenga tabia ya kusoma vitabu ili kuwa na uelewa mpana wa masuala mbalimbali ya kisanyansi na kijamii ili kupata maarifa na kujiwekea mazingira mazuri ya ufaulu wa mitihani ya kumaliza elimu ya msingi.

Muasisi na Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe Foundation ,Jacqueline Mengi alisema hayo hivi karibuni mara baada ya kuzindua maktaba yenye vitabu vya kitaaluma na hadhithi alivyokabidhi kwa uongozi wa shule ya msingi Uhuru kwa ajili ya kuwawezesha wanafunzi kujisomea nyakati za masomo shuleni hapo.

Alisema ,lengo la Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe Foundation ni kuhimiza watoto hususani wanafunzi kupenda kujisomea vitabu ili kujenga maarifa na msingi wa maisha katika siku za usoni.

“Taasisi inazindua maktaba ya shule ya Msingi Uhuru ya Manispaa ya Morogoro na inawahusu wanafunzi wote ili wasome vitabu kwa ajili yakujenga uelewa na wasisome kwa ajili ya kufauli mtihani bali kila siku “ alisema Mama Mengi.

Muasisi na Mkurugenzi mkuu huyo alisema ,tangu kuanzishwa kwa Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe Foundation ,hiyo ni mara ya kwanza kuweza kufungua maktaba ya vitabu kwa shule ya msingi nje ya mkoa wa Dar es Salaam.

Alisema ,Taasisi hiyo ina unga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya tano katika masuala ya uboreshaji wa elimu na kwa kufanya hivyo imeweka mpango endelevu wa kufungua maktaba za vitabu kwa shule za msingi nje ya mkoa huo wa Dar es Salaam.

“  Nimefurahi kuona tumeanza kupiga hatua kubwa , lengo la Taasisi ni kufungua maktaba za vitabu kila mkoa nchini na ikiwezekana hadi ngazi ya kila wilaya ili kila shule inakuwa na maktaba iliyoanzishwa na Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe “ alisema mke wa Mengi .

Naye Mkuu wa shule ya Msingi Uhuru iliyopo Kata ya Uwanja wa Taifa,Manispaa ya Morogoro, Muchunguzi Lutagwelera , alimpongeza mama Mengi na Taasisi yake kwa kuona umuhimu wa kuisaidia shule hiyo kukarabati chumba cha darasa na kufungua maktaba ya vitabu kwa ajili ya kujisomea wanafunzi na kuwawezesha kuongeza kiwango cha ufaulu.

Alisema , shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 1971 hadi sasa ina wanafunzi 1,651 kati hayo wavulana 844 na wasichana 807 na licha ya changamoto kadhaa imekuwa ikifanya vizuri katika mitihani ya darasa la nne na la saba kuwa katika kumi bora kwenye shule za msingi za Manispaa ya Morogoro.

Nao wanafunzi wa shule hiyo katika risala yao kwa mgeni rasmi iliyosomwa na dada wa shule , Regina Julias pamoja na kutoa shukrani nyingi kwa Taasisi ya Dr Ntuyabaliwe Foundatin kwa kuweza kuichagua shule yao kuiwezesha kuwa na chumba cha Maktaba.

“ Tunaahidi tunaitunza maktaba hii pamoja na vifaa vyote vilivyomo ili viweze kudumu na kusaidia wanafunzo wote hata wale ambao hawajaanza shule “ alisema Regina.

Hata hivyo walimwomba awe mlezi wa shule hiyo na kushirikiana na uongozi wa shule katika kuondoa kero kubwa ya uzio , madarasa , matundu ya vyoo na samani .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa