• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

UMEME WALETA NEEMA KWA WAGONJWA NA WAJAWAZITO WANAOJIFUNGUA ZAHANATI YA TOWELO, MANISPAA MOROGORO

Posted on: August 13th, 2018

Tatizo la wanawake wajawazito kujifungua kumulikiwa taa ya kandili na kurunzi za simu katika Zahanati ya Towelo ,iliyopo Manispaa ya Morogoro litabaki historia mara baada ya Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO), mkoa wa Morogoro kupeleka umeme ukiwa ni utekelezaji wa agizo la Naibu Waziri wa Nishati .

Naibu Waziri wa Nishati , Subira Mgalu , machi mwaka huu aliitembelea Zahanati hiyo iliyojengwa katika safu ya milima ya Ulunguru ambapo alijionea haina umeme na kutoa agizo hilo kwa Shirika hilo kufikishia umeme .

Katika ziara hiyo viongozi mtaa wa Towelo na wananchi waliwasilisha malalamiko kwa Naibu Waziri juu ya changamoto wanazozipata hasa wanawake wajawazito kumulikiwa na taa za kandiri na kurunzi za simu wakati wa kujifungua.

Hata hivyo Naibu Waziri huyo hivi karibuni akiwa wilayani Morogoro aliitembelea tena Zahanati hiyo kwa ajili ya kuona utekelezaji wa agizo lake na alipofika alikuta umeme ukiwa unawaka.

Akiwa katika Zahanati hiyo , Naibu waziri aliwataka wauguzi na wakunga kuwahudumia wananchi kwa kukaa muda wa saa 24 katika Zahanati hiyo kwa vile kisingizio cha haina umeme sasa kimeondolewa .

Naye Mjumbe wa kamati ya zahanati hiyo, Siajabu Abeid akizungumza mbele ya Naibu Waziri mara baada ya kufikishwa kwa umeme katika Zahanati hiyo alisema, huduma za matibabu zinatolewa saa 24 tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo usiku ilikuwa ikifungwa .

Alisema, uwepo wa umeme katika Zahanati hiyo ,kumeondoa changamoto iliyokuwa ikiwakabili wagonjwa ya kukosa vipimo vinavyotumia umeme vikiwemo vya malaria.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa agizo la Naibu Waziri, Kaimu meneja wa Tanesco mkoa wa Morogoro Mhandisi Lawrence Maro alisema, upelekaji umeme katika Zahanati hiyo umegharimu zaidi ya Sh. 54 milioni fedha ambazo zilitokana na vyanzo vya ndani.

Mhandisi Maro alisema, kutokana na ukubwa wa transfoma waliyoiweka wameweza pia kupeleka umeme huo katika shule ya msingi ya Towelo iliyopo katika eneo hilo.

Katika hatua nyingine Naibu waziri huyo pia alizindua uwashaji umeme katika kijiji cha Mtego wa Simba kilichopo Kata ya Mkambalani , halmashauri ya Wilaya ya Morogoro utakaosambazwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Alisema, katika bajeti iliyopitishwa hivi karibuni , mkoa wa Morogoro umetengewa kiasi cha Sh: Bilioni 45 kwa ajili ya kujenga miundombinu na kusambaza umeme kwenye vijiji 150 kupitia mradi wa Rea. .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa