• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

UWT WAADHIMISHA MIAKA 47 YA CCM KWA KUWASAIDIA WAATHIRIKA WA MVUA MOROGORO MJINI

Posted on: January 29th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro mheshimiwa Rebecca Nsemwa, leo tarehe 29.01.2023 amepokea msaada wa chakula, sabuni, na mavazi kutoka kwa Kamati ya Maafa yaUmoja   wa   Wanawake   wa   Tanzania   (UWT)   mkoa   wa Morogoro,   msaada   uliolengakuwafariji   wananchi wa Manispaa  ya   Morogoro,   waliopatwa na maafa kutokana na mvua nyingi zinazoendelea kunyesha.

Mara   baada   ya   kupokea   msaada   huo, mheshimiwa Nsemwa   amewashukuru wananwake   wa   (UWT) mkoa   wa   Morogoro   kwa   tendo   hilo jema   walilofanya,   kishaakatoa   wito   kwa   watu   mbalimbali,   taasisi   na   mashirika   yaliyomo   ndani   na   nje   ya Morogoro kujitokeza kuwasaidia   wananchi   walioathiriwa   na   mvua   zinazoendelea kunyesha kwani msaada kama huo wa chakula na mavazi unahitajika sana kwao kwa sababu maafa ni jambo ambalo mtu hapangi limkute.

Mheshimiwa   Nsemwa   ametoa   wito   kwa   wananchi   ambao   bado   wanaishi kwenye maeneo ambayo  ni mikondo ya maji, waondoke kwenye  maeneo hayo kwani  mvua bado zinaendelea kunyesha na huenda zikaunganisha na mvua za masika, hivyo ni vyema kuendelea kuchukua tahadhari kwa kuhama kwenye maeneo yote hatarishi.

Aidha, mheshimiwa Nsemwa amevipongeza vikosi vya uokoaji vya Wilaya kwa msaada mkubwa uliosaidia wananchi kuwa salama, walioutoa siku chache zilizopita baada ya maji kuathiri makazi ya watu na mali zao. 

“Juzi vikosi vyetu vya uokoaji viligawana maeneo ya kufanya uokoaji na hii ilisaidia sana  wananchi   wetu   kuwa salama.   Lakini   pia   tunashukuru kwamba   mvua ilinyesha mchana   huenda   ingenyesha   usiku   maafa   yangekuwa makubwa   zaidi.   Ninawasihi wananchi   katika   kipindi   hiki, punguzeni   safari   za   usiku   zisizokuwa   za   lazima,   na mnapofikwa na majanga msipaniki bali kuweni watulivu na mpige simu Ofisini kwangu ili tuweze kuwapatia  msaada   wa   uokozi   kupitia vikosi  vyetu   vya   uokoaji. Mkipaniki na kuanza kukimbia huku na kule mnaweza kusombwa na maji” alieleza Nsemwa.

Kwa upande wake Katibu wa UWT mkoa wa Morogoro, ndugu Mwajabu Ally Maguluku,ambaye ndiye alikabidhi msaada huo kwa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, amesema msaada walioutoa una thamani isiyo pungua shilingi laki tano za Tanzania, na kwamba imekuwa ni desturi   yao   kutoa   misaada kama hiyo katika   kipindi   hiki ambapo awali, walifanya hivyo kwa maeneo ya Kilosa, Hanang, na Mvomero.

Amesema   Wanawake   wa   UWT   wataendelea   kuchangishana   ili   kuendelea   kuleta msaada kwa waathirika wa ndani ya Manispaa ya Morogoro. Lakini pia amemshukuru mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Mheshimiwa Abood kwa kuwa tayari kuwapatia usafiri kila mara wanapohitaji kwenda mahali fulani kupeleka misaada kwa waathirika wa mvua.

Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT), wametoa msaada huo ikiwa ni namna yaoya kuadhimisha miaka 47 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa