• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

VIJANA TUMIENI FURSA YA UWEZESHAJI WA MIKOPO INAYOTOLEWA NA HALMASHAURI KUJIKWAMUA KIUCHUMI

Posted on: August 29th, 2022

WATANZANIA wakiwemo vijana nchini wameshauriwa kuchangamkia fursa za uwezeshaji wa mikopo inayotolewa na Serikali kupitia Halmashauri za wilaya , Manispaa na Majiji ili waanzishe miradi ya ujasiliamali ya kujikwamua na umaskini wa kipato.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2022 , Sahil Geraruma alitoa rai hiyo katika Kata ya Mazimbu Manispaa ya Morogoro baada ya Mwenge wa Uhuru kupitia kuona mradi wa kikundi cha vijana wa Chama cha Mafundi Ujenzi.

Geraruma alisema , Serikali ya awamu ya sita inawajali wananchi wake kwa kutoa fursa mbalimbali zikiwemo za mikopo isiyo na riba kwa makundi ya vijana , wanawake na watu wenye ulemavu kupitia fedha zinazotolewa na Halmashauri za wilaya, Manispaa na Majiji.

“ Kwanza kabisa naomba niwafikishie habari njema vijana , kuna asilimia 10 zinazotokana na makusanyo ya fedha za ndani za Halmashauri na asilimia hiyo imegawanyika makundi matatu asilimia nne kwa vijana umri kuanzia miaka 18 hadi 35 “ alisema Geraruma

Alisema wanachopaswa ni kufuata utaratibu wa kuunda vikundi , kusajili kikundi , kuunda katiba ya kikundi kwa kuzingatia sheria ndogo ndani ya Halmashauri husika , kufuata taratibu zote kwenye Ofisi ya Maendeleo ya Jamii na ya mkurugenzi mtendaji na kwamba mkopo huo hauna riba.

Geraruma alitaja kundi lingine la wanawake ambalo lina asilimia nne na kwamba utaratibu ni kuunda vikundi vya watu kuanzia watano na  kuwekewa ukomo wa umri ni kuanzia miaka 18 na kuendelea.

Kundi lingine linalonufaika na mkopo huo ni la watu wenye ulemavu ambalo limetengewa asilimia mbili pia kwa utaratibu wa kuunda vikundi lakini wao hata mtu mmoja mmoja anaweza kukopeshwa.

“ Kwa hiyo ndugu zangu Rais ametoa fursa tuweza kunufaika nayo , watanzania wenzangu zingatieni fursa hiyo ili tuweze kunufaika , tusikae mitaani tukaanza kulalamika kila wakati maisha magumu ..maisha magumu wakati kuna fursa Rais ametoa na hatujazitumia “ alisema Geraruma

Aliwataka vijana kuchangamkia fursa hiyo kwa kufuata utaratibu uliowekwa kupata mikopo isiyo na riba ili iwawezeshe kuanzisha shughuli mbalimbali za kiuchumi ambazo zitawasaidia kuboresha maisha yao na pia kukuza uchumi wa Taifa .

Pamoja na hayo aliwataka wanufaika mikopo hiyo kurejesha kwa wakati ili endelee kutolewa kwa wezao mwengine na kwamba endapo kutajitokeza changamoto za kuchelewa kurejesha wanapaswa kuwasiliana na viongozi wa ngazi ya Halmashauri kutatua changamoto hizo.

Geraruma pia alitumia fursa hiyo kuipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kupitia Mkurugenzi wake kutenga fedha za asilimia 10 zitokanazo na mapato ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo kwa makundi ya wanawake , vijana na watu wenye ulemavu.

Awali Katibu wa Kikundi cha vijana wa Chama cha Mafunzi Ujenzi , Annastazia Charles akitoa taarifa ya mradi huo kwa Kiongozi wa mbio cha Mwenge wa Uhuru alisema kikundi kilianzishwa mwaka 2018 kikiwa na wanachama 11 ambapo wavulana ni tisa na wasichana wawili na kilipata usajili wa Manispaa mwaka 2020.

“ Kikundi hiki kinajishughulisha na kufyatua matofali mchanganyiko wa saruji na mchanga (blocks) kwa kutumia mtambo wa kushindilia mchanga na saruji” alisema Annastazia

Alisema mwaka 2021/2022 kikundi kilipata mkopo wa Sh milioni 24 ikiwa ni sehemu ya mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya  ndani ya Manispaa kwa makundi ya ( wanawake, vijana na watu wenye ulemavu )na fedha hizo zilitumika kununua mashine mbalimbali na vifaa vya kufyatua matofali katika mradi huo .

Annastazia alisema hasi sasa mradi huo una thamani ya Sh milioni 39.2 ambazo Sh milioni 24 ni mkopo kutoka Halmashauri ya Manispaa hiyo na Sh milioni 15.2 ni mchango wa wanachama ukiwa ni mtaji wa kikundi chenyewe na mradi umekamilika na unatoa huduma.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa