• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WAAJIRI SEKTA BINAFSI RUHUSUNI WATUMISHI WENU KUJIUNGA NA CHAMA CHA WAFANYAKAZI - RC MALIMA.

Posted on: May 1st, 2025

MKUU wa Mkoa wa Morogoro,Mhe.Adam Malima,ametaka waajiri hasa wa Sekta binafsi kuwaruhusu waajiriwa wao ili waweze kujiunga na Chama cha Wafanyakazi chochote ili waweze kunufaika na kuzisaidia sekta zenu kwakuwa ni wajibu na haki kwa pande zote mbili.

Kauli hiyo ameitoa katika kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani (MEI MOSI) ambayo kwa Mkoa wa Morogoro sherehe zilifanyika katika Uwanja wa Mpira wa miguu wa Jamhuri Morogoro Mei 01-2025.

"Pamoja na kuwapongeza kwa maadhimisho haya leo, nichukue nafasi kuwaelekeza waajiri wote wa Sekta binafsi kuwaruhu watumishi wao kuchagua Chama cha Wafanyakazi chochote na kujiunga kwakuwa ni haki yao nanyi ni wajibu wenu kutekeleza hili," Amesema RC Malima.

RC Malima amewaahidi wafanyakazi wa Mkoa wa Morogoro kuwa yale yote yaliyosemwa na viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi Mkoa ameyachukua na kwa yale yaliyo ndani ya uwezo wake atayatekeleza haraka na kwa ufanisi zaidi, na kwa yale yaliyo juu ya mamlaka yake ameahidi kuyafikisha tena kwa maandishi bila kupunguza neno lolote.

Kuhusu suala la Kikokotoo, RC Malima , amesema kuwa ni jambo ambalo kwa hivi karibuni limesemwa na mamlaka mbalimbali na hivyo anayoimani kubwa na Serikali kuwa litafanyiwa kazi na pande zote zitakuwa sawa kabisa kwakuwa Serikali ya Dkt.Samia Suluhu Hassan hii ni sikivu sana.

Aidha,amewataka waajiri kushughulikia haraka mafao ya watumishi wastaafu bila usumbufu huku akiwataka Ofisi ya Kazi Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na OSHA kupeleka majina katika Ofisi yake kwa Taasisi ambazo zinakiuka misingi ya kazi pamoja na usalama wa wafanyakazi kazini.

Katika hatua nyingine,amewataka waajiri kufuata sheria za kuwaajibisha watumishi kwani kutofuata sheria ni ukiukwaji wa misingi ya utawala bora na unaweza kuisababishia hasara Serikali.

Pia,ametoa wito kwa waajiri kupeleka fedha za watumishi kwenye mifuko ya hifadhi na kuhakikisha suala la madeni ya watumishi linafanyiwa kazi na yeye Ofisi yake itakuwa mstari wa mbele kufuatilia hilo.

Kauli Mbiu ya Mei Mosi Kitaifa 2025 imebeba ujumbe wa " Uchaguzi Mkuu wa 2025 Utuletee Viongozi Wanaojali na Kuthamini Haki na Maslahi ya Wafanyakazi" Ewe Mfanyakazi Shiriki.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • BALOZI BATILDA ATAKA MAONI YA WADAU KUFANYIWA KAZI KUELEKEA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MSHARIKI 2025

    May 06, 2025
  • MAAFISA ARDHI WATAKAOBAINIKA NI VYANZO VYA MIGOGORO YA ARDHI TUTAWAFIKISHA MAHAKAMANI-DKT.NDUMBARO.

    May 05, 2025
  • WAAJIRI SEKTA BINAFSI RUHUSUNI WATUMISHI WENU KUJIUNGA NA CHAMA CHA WAFANYAKAZI - RC MALIMA.

    May 01, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa