• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WABUNGE WA MOROGORO MJINI WATOA HOJA KWENYE KAMATI YA USHAURI YA WILAYA

Posted on: February 19th, 2024

Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, mheshimiwa Abdul-Aziz Abood na Mbunge wa Viti Maalum wa jimbo hilo, mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma wamehudhuria na kutoa mapendekezo kwenye kikao maalum cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Morogoro, kilichofanyika tarehe 19.02.2024 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Manispaa hiyo, kwa lengo la kujadili bajeti ya Manispaa ya Morogoro.

Mbunge Abood amempongeza Mkuurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kwa kukamilisha miradi mingi viporo aliyoikuta ndani ya Manispaa miaka miwili iliyopita kisha akashauri uwekezaji zaidi kwenye rasimali watu na vitendea kazi katika sekta ya afya.

“Ndugu Mkurugenzi asante sana kwa ushirikiano wako tumetekeleza ujenzi wa Zahanati na Vituo vya Afya. Sasa tufikirie kuongeza rasilimali watu kwenye maeneo hayo ili wananchi wetu waweze kupata huduma za afya kwa wakati” alieleza mheshimiwa Abood.

Mheshimiwa Ishengoma naye amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa kwa utendaji wake mzuri kisha akamshukuru Rais Samia kwa fedha nyingi za maendeleo ambazo amezileta ndani ya Manispaa ya Morogoro hata kufanikisha miradi mbalimbali kutekelezwa hasa katika sekta za afya na elimu.

Pia, mheshimiwa Ishengoma amesema amefurahi sana kuona jengo dogo la upasuaji (mini-thietre) linajengwa kwenye kituo cha afya cha Sabasaba kwani huduma za upasuaji zitakapoanza kutolewa kituoni hapo itakuwa ni mkombozi kwa wanawake hasa wale wanaopata matatizo wakati wa kujifungua.

“Wanawake wengi wanapenda kujifungulia kwenye kituo cha afya cha Mafiga na SabaSaba hivyo naomba sana ujenzi wa jengo la upasuaji usimamiwe vyema na ukamilishwe haraka” aliongeza kusema mheshimiwa Ishengoma.

 Aidha, mheshimiwa Ishengoma ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa kwa bajeti nzuri iliyowasilishwa na kutoa rai kwamba isimamiwe vyema kusudi Manispaa iweze kukua na hatimaye kukidhi vigezo vya kuwa jiji.

Nao wajumbe wa kikao hicho wakiwemo viongozi wa vyama mbalimbali vya Siasa, na viongozi wa dini wameipongeza ofisi ya Mkurugenzi kwa kuandaa bajeti nzuri kisha wakatoa maoni yao katika sekta za elimu, afya, uchumi, usalama, na miundombinu, maoni ambayo mkurugenzi wa Manispaa, ndugu Ally Machela ameahidi kuyafanyia kazi na kuyaingiza kwenye mpango wa bajeti iliyowasilishwa.

Kwa mujibu wa Mchumi wa Manispaa, ndugu Jeremiah Lubeleje, bajeti ya Manispaa ya mwaka wa fedha 2024/2025 imekisiwa kupanda kwa asilimia 18.8 huku ndani yake kukiwa na miradi 12 ya kimkakati, miradi vipaumbele 18 ya sekta za elimu, afya, utawala, uchumi, ardhi, na miundombinu.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, ndugu Ally Machela ameieleza Kamati hiyo hatua za kimaendeleo ambazo Manispaa imeweza kupiga ndani ya miaka miwili ya uongozi wake, ikiwemo kukamilisha miradi viporo katika sekta za elimu na afya, kujenga Zahanati 10 ambazo saba kati yake yatari zinafanya kazi na tatu zinatazamiwa kuanza kufanya kazi kabla ya mwezi wa sita waka huu, kujenga vituo vya afya Lukobe na Tungi, na kupandisha hadhi Zahanati ya Mazimbu kuwa kituo cha afya.

Hatua nyingine ni kujenga shule nane za Sekondari kwenye kata ambazo hazikuwa na shule hivyo kufanya idadi ya kata zisizokuwa na shule ya sekondari kuwa ni mbili tu kati ya kata zote 29 za Manispaa.

Vilevile, ndugu Machela amesema katika kuboresha sekta ya elimu msingi, Manispaa imejenga shule mbili mpya kwenye kata ya Mindu na Mafisa, na katika ardhi migogoro zaidi ya elfu tatu imetatuliwa, na bajeti ya mapato ya ndani ya Manispaa imepanda kutoka bilioni 10 miaka miwili iliyopita hadi bilioni 16 sawa na ongezeko la bilioni 5.6.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa