• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WAFANYAKAZI WA MKOA MORO WAMPONGEZA JPM KUREJESHA KIKOKOTOO CHA ZAMANI .WAMUOMBA ATUPIE JICHO LA HURUMA MIFUKO YA SEKTA BINAFSI

Posted on: January 12th, 2019

Wafanyakazi shiriki wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) mkoa wa Morogoro wamemuomba Rais Dk John Magufuli atupie jicho lake lenye huruma kwenye mifuko ya mafao yanayotolewa na mifuko ya sekta binafsi nchini kwani ni kidogo na kikokotoo cha asilimia 25 inalenga wafanyakazi sekta binafsi.

Kwani mishahara ya wafanyakazi hao ni duni kiasi kwamba , kwa mujibu wa kikikotoo cha asilimia 25 , wastaafu wa sekta hizo , bado watendelea kuumia kwa kulipwa mafao kidogo licha ya usawa katika uchangiaji.

Hayo yalibainishwa katika risala ya wafanyakazi wa TUCTA mkoa wa Morogoro ambayo iliyosomwa na Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Morogoro , Aboubakar Mpimbi mbele ya Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen Kebwe.

Mkuu wa mkoa huyo alikuwa mgeni rasmi kupokea maandamano ya amani ya wafanyakazi wa  vyama shiriki vya Tucta ya kumpongeza Rais Dk John Magufuli kwa kurejesha kikokotoo cha zamani cha mafao ya wastaafu

. Mpimbi alisema, Tucta mkoa wa Morogoro kwa niaba ya wafanyakazi wote wa mkoa huo wanatoa pongezi zao za dhati kabisa kwa Rais kwa kukubali kupokea kilio cha wafanyakazi cha kulalamikia kikokotoo kipya cha mafao ya kustaafu cha mwaka 2018 na kukisimamisha kwa muda kisitumike kwa sasa.

“ Tunaendelea kumpongeza kwa dhati kabisa kwa kurejesha kanuni ya kikokotoo cha zamani hadi kufikia mwaka 2023” alisema Mpimbi kupitia risala hiyo.

Kupitia risala hiyo alisema , Tucta mkoa wa Morogoro wameendelea kumwomba Rais aendelee kuingilia kati mienendo ya kiutendaji ya mifuko hiyo ili itoe mafao yenye tija kwa wanachama wake na kwa usawa kwa sababu nia ya serikali ya awamu ya tano ni kuona wanachama wa mifuko wananufaika na mifuko yao.

Akiongea mara baada ya kupokea maandamano hayo Mkuu wa Mkoa Dk Kebwe amewataka wafanyakazi kuiishi na kauli mbiu ya Rais ya “hapa kazi tu” kwa kufanya kazi kwa bidii, uaminifu na nidhamu ya hali ya Juu.

Hata hivyo aliwataka wafanyakazi  wajipange kufanya kazi kwa bidii ili tija iweze kuonekana na kutumia fursa za mikopo inayotolewa na Tasisi za Umma za kifedha kupata mikopo ikiwemo ya mabenki ili iwasaidie kuanzisha miradi ya ujasiriamali na kilimo ili kuendeleza uchumi wao kabla ya kustaafu.

“ Kikokotoo hiki kiwe ni ziada ya kumwezesha mstaafu kuishi vizuri , lakini ukijandaa ukiwa kazini ni jambo jingine la muhimu “ alisema Dk Kebwe.

Katika hatua nyingine aliwaagiza viongozi wa TUCTA mkoa  kumpelekea orodha ya taasisi na makampuni yasiyoingiza wafanyakazi wake kujiunga na mifuko ya hifadhi ili aweze kuyachukulia hatua za kisheria kupitia Ofisi ya Waziri mkuu kwani kutofanya hivyo ni kukiuka sheria za nchi na kuwanyonya wafanyakazi.

Kwa upande wao Mwenyekiti wa TUCTA Mkoa wa Morogoro Mohamed Simbeye pamoja na Mwenyekiti wa Wanawake cha Chama cha Tpawu mkoa wa Morogoro, Lukia Merey kwa nyakati tofauti walimpongeza Rais kwa kurejesha kikokotoo cha zamani .

Hata hiyo walimwomba pia aendelee kuangalia namna ambayo kikokotoo hicho kutoishia mwaka 2023 bali kiwe endelevu hata baada ya mwaka 2023 na kundi la wafanyakazi wa sekta binafsi kiweze kuongezeka angalao kwa asilimia 40 au 50 sawa na wenzao .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa