• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WAITARA ARIDHISHWA NA USAFI MANISPAA YA MOROGORO, ATAKA KASI IONGEZWE KATIKA UPATIKANAJI WA DAMPO LA KISASA

Posted on: January 25th, 2021

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mwita Waitara, ameipongeza Manispaa ya Morogoro kwa mipango mizuri na usimamizi mzuri wa usafi huku akitaka nguvu iongezwe katika ufuatiliaji wa upatikanaji wa dampo la Kisasa.

Kauli hiyo ameitoa  wakati wa ziara ya ukaguzi wa dampo la taka Manispaa ya Morogoro lililopo Kata ya Mafisa.

''Nimefurahishwa sana na hatua za kuanza kutekeleza ujenzi wa dampo la Kisasa, mmeniambia tayari andiko lipo na mshaliwasilisha kazi yangu mimi ni kusukuma ili hizo fedha zitoke, lakini niwaombe dampo la kisasa lizingatie miundombinu yote, lisiwe kama hili la kienyeji,mhakikishe mnajiandaa vyema na ujenzi  wa dampo Jipya , hili tulilo nalo tuliwekee mazingira rafiki taka zisibaki nje, hapa kuna taka ambazo zinazalisha sumu, haya maji yakitiririka yanawafikia wananchi na ni hatari kwa afya"Alisema Waitara.

Aidha, amesema sio jambo baya Manispaa ikafanya ziara kwa ajili ya mafunzo na kuona wenzenu walivyojipanga katika ujenzi wa madampo pia  usafishaji wa Mji .

Mhe. Mwita, amesema kutohudumia dampo hilo ipasavyo kunapelekea uchafuzi wa mazingira, harufu mbaya, na maji yenye sumu kali na kuhatarisha afya ya wakazi wa maeneo jirani viumbe hai na mazingira kwa ujumla.Aidha alisisitiza kuendelea kutoa elimu kwa wananchi  jinsi ya kutenganisha taka nyumbani ili waone taka ni dili na sio uchafu mara baada ya kuanzisha kiwanda chenu cha uchakataji wa takataka.

Katika ziara hiyo ameitaka Halmashauri kuwa na mikakati mizuri ya kusimamia usafi ikiwa ni kuwa na mbinu bora za kufanya kila mmoja kuona jukumu la usafi ni lake na kuwa na sheria ambazo zitatekelezwa kwa asilimia mia moja katika usafi ikiwa ni pamoja na tozo za usafi na faini kwa wale waharibifu wa mazingira.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Bakari Msulwa, amesema Wilaya ya Morogoro inakabiliwa na changamoto nyingi za kimazingira lakini wapo tayari sasa kuanza kutekeleza maagizo hivyo watajipanga na timu ya wataalamu kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkoa na NEMC ili kuona changamoto hizo zinafanyiwa kazi.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, amesema wapo katika hatua za kuhakikisha kwamba Kamati zote za Mazingira zinafanya kazi ipasavyo ili kuondokana na tatizo hilo.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba,amesema Manispaa ya Morogoro imetenga bajeti ya shilingi milioni 300 kwa ajili ya ununuzi wa gari la taka ili kuongeza nguvu katika uondoaji wa taka.

Awali akitoa taarifa ya hali ya mazingira na usimamizi wa taka katika Dampo, hilo, Afisa anayesimamia Dampo, Alex Roman, , amemueleza Mhe. Waitara kuwa, Dampo hilo linakabiliana na changamoto mbali mbali ikiwa ni pamoja dampo kutokuwa la kisasa , idadi ya watu wanaongezeka pamoja na uzalishaji wa taka katika Kiwanda cha Mpunga.

Romani, amesema, kwa siku Dampo hilo linapokea tani 180 hadi 200 za taka zinazozalishwa na kuingia katika dampo hilo.

Amesema katika kuhakikisha changamoto hiyo inakwisha, Manispaa ya Morogoro imeandaa eneo Kiegea lenye zaidi ya hekari 1000 ili kujenga Dampo la kisasa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa