• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WAMILIKI WA ARDHI NA VIWANJA ‘WASIOJULIKANA’ MORO MAJINA YAO YATAMBULIWE. WALIPE KODI.

Posted on: October 18th, 2017

NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi , Angelina Mabula amemwagiza Mkurungezi wa Manispaa ya Morogoro, John Mgalula kufuatilia kwa karibu majina ya wamiliki wa ardhi na viwanja wasiojulikana kwenye mfumo wa ukusanyaji wa mapato kielektroniki na wanadaiwa kukwepa kulipa kodi ya ardhi na kuikosesha mapato Serikali.

Naibu Waziri alitoa agizo hilo alipofanya ziara ya siku moja aliyoifanya Oktoba 17, 2017 katika Manispaa ya Morogoro na kutembelea Ofisi za Ardhi Manispaa hiyo ambayo ilikuwa na lengo la kujionea maendeleo ya mfumo wa ukusanyaji kodi ya ardhi kwa njia ya kielektroniki.

Mbali na kuagiza ufuatiliaji wa majina ya wamiliki hao pia alimtaka Mkurugenzi  kutoa maelezo ya kina kuhusiana na majina ya wamiliki wa ardhi kutoonekana katika mafaili yao licha ya nyaraka nyingine muhimu kuwemo.

Katika ukaguzi wake na kuangalia mfumo huo, Naibu Waziri huyo alibaini kuwepo kwa mapungufu makubwa ya uhifadhi wa nyaraka , ikiwemo kufichwa kwa baadhi ya majina ya wadaiwa, ambao wanaonekana hawajalipa kodi ya ardhi kwa muda mrefu.

Naibu Waziri alijionea mafaili zaidi ya 300 ambayo majina hayakuingizwa  katika mfumo yakisomeka ‘Ndugu Mhusika’ ambao ni wadaiwa sugu waliolimbikiza madeni kuanzia kiasi cha Sh milioni moja hadi kufikia milioni 25.

“ Nimebaini katika ukaguzi wangu kuwa baadhi ya wateja hawajulikani majina na wameandikwa kwenye mafaili yao ‘ Ndugu Mhusika ‘ ni watu wasiojulikana ingawa kwenye mafaili yao kuna nyaraka za vipimo vya ardhi ya viwanja na nyinginezo isipokuwa hawana majina” alishangazwa Naibu Waziri Mabula.

“ Alimwagiza  Mkurugeni watu hao wajulikane majina yao na walipe malimbikizo ya kodi ya ardhi kwa mujibu wa sheria na kuhahidi kupita tena muda mfupi ujao kuona iwapo agizo hili limetekelezwa” alisema Naibu Waziri.

Naibu Waziri alisema , sekta ya ardhi imeachiwa kwa wataalamu wa ardhi na kitendo kinachowafanya baadhi ya Wakurugenzi wa halmashauri za miji, wilaya , Manispaa na Majiji kushindwa kufahamu idadi kamili ya viwanja katika maeneo yao na jambo hilo linatoa mwanya wa udanganyifu wa viwanja na kukosesha mapato serikali.

Pamoja na hayo Naibu Waziri huyo alizitaka Halmashauri zote zilizopo mkoani Morogoro kutatua changamoto mbalimbali zilizopo kwenye sekta ya ardhi na kuweka ya matumizi bora ya ardhi na upimaji wa maeneo ya makazi na mashamba.

Kwa upande wake Ofisa Ardhi Mteule Manispaa ya Morogoro , Matilda Maktavo alisema, baadhi ya maeneo tayari yameanza kufanyiwa uhakiki, kabla ya kuingizwa kwenye mfumo wa kieletroniki, ili kupata taarifa zilizo sahihi za wateja.

Alisema kuwa mapungufu madogo madogo yaliyojitokeza ni wakati wa uhamishaji wa taarifa kutoka mfumo wa zamani kwenda wa Kieletroniki na hali hiyo inafanyiwa kazi .

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro , John Mgalula alimhakikishia Naibu Waziri kuwa kasoro na changamoto zilzojitokeza wakati wa uhamishaji wa nyaraka kuingizwa kwenye mfumo wa kieletroniki zinafanyiwa kazi kwa ukamilifu ili kutimiza lengo ya ukusanyaji wa mapato ya serikali.

Hata hivyo alisema , Naibu Waziri huyo katika ziara hiyo amewezesha kutoa somo na kufundisha namna ya uendeshaji wa mfumo huo na kutunza nyaraka na kwamba hakuja kumtafuta mchawi bali ni kuelekeza namna ya uboreshaji wa utendaji wa kazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa