• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WANANCHI WAASWA KUKAMALIZIA MALIPO YA ZOEZI LA URASIMISHAJI WA MAENEO YAO KWANI LIMEKARIBIA UKINGONI

Posted on: July 18th, 2023



WANANCHI wa mtaa wa Napome Kata ya Chamwino wametakiwa kuongeza bidii katika kulipia huduma ya urasimishaji wa mtaa wao ili waweze kupata hati na kuepuka migogoro ya ardhi.

Rai hiyo imetolewa leo tarehe 18.07.2023 na Afisa Ardhi wa Manispaa ndugu Valency Huruma wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa mtaa huo waliokuwepo kwenye ofisi ya Kata ya Chamwino wakati Kamati ya Mipangomiji na Mazingira ya Manispaa ilipotembelea mtaa huo ili kuona maendeleo ya zoezi la urasimishaji wa mtaa huo.

“Zoezi la urasimishaji lilipewa kipindi cha miaka 10 hadi kukamilika kwake na mwaka huu ndio wa mwisho hivyo tumieni fursa hii ambayo ni kama ofa ambayo serikali imeitoa kwa wananchi wake nchi nzima mkamilishe malipo ili mpate hati zenu” alifafanua Afisa Ardhi Valency.

Naye Mkandarasi wa Kampuni ya Urasimishaji ya Lunda Ardhi Consult inayotekeleza zoezi hilo la Urasimishaji wa Mtaa wa Napome amesema mpaka sasa kila kiwanja cha mtaa huo tayari kina bikoni na ramani za maeneo yote yaliyopimwa zipo lakini changamoto iliyopo ni kwamba wananchi bado wanaendelea kumegeana kiholela maeneo ya viwanja vyao ambayo tayari yamekwisha kurasimishwa na kati ya viwanja 400 vilivyopimwa na kurasimishwa viwanja 100 tu ndio ambavyo mpaka sasa vimekwisha kulipiwa, hali ambayo inapelekea kukwama kwa ukamilishaji wa zoezi lililobaki la kutoa michoro na kuwapatia watu namba za viwanja vyao.

Hivyo Mwenyekiti wa Kamati ya Mipangomiji na Mazingira ya Manispaa, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mwembesongo, Mheshimiwa Ally Rashid Kalungwana,akawaasa wananchi wa mtaa wa Napone kuhamasishana wao kwa wao na kuongeza kasi ya kulipia zoezi hilo la urasimishaji wa mtaa wao ili waweze kupata hati na namba za viwanja vyao.

Aidha, wananchi  waliohudhuria katika kikao hicho waliomba elimu zaidi kuhusu bikoni ambazo tayari zimekwisha kupandwa katika viwanja vyao na baada ya kupewa elimu hiyo waliridhia kuongeza kasi ya kulipia zoezi hilo hili waweze kupatiwa namba za viwanja na hati zao.

MWISHO


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa