• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WANAWAKE MORO WAHIMIZWA KUANZISHA VIKUNDI VYA UJASIRIAMALI WAJIINUE KIUCHUMI

Posted on: March 31st, 2018

Wanawake mkoani Morogoro wamehimizwa kufanya kazi kwa bidii na kuacha kuwategemea kwa asilimia kubwa wanaume zao na badala yake waungane kuanzisha vikundi vya ujasiriamali vikiwemo vya viwanda vidogo ili kuinua uchumi wa familia na taifa kwa ujumla.

Ofisa ustawi wa Jamii, Sidina Mathias alisema hayo hivi karibuni katika shule ya msingi Azimio iliyopo kata ya Kihonda katika Manispaa , ukiwa ni mwendelezo wa siku ya wanawake duniani ambayo iliandaliwa na Taasisi isiyo ya kiserikali  ya Maendeleo ya Jamii (HACOCA) kwa kushirikiana na Taasisi isiyo ya kiserikali ya RIGHT TO PLAY.

Alisema kuwa, endapo wanawake wanajitoa kujiunga kwenye vikundi vya ujasiriamali hasa viwanda vidogo wanaweza kujikwamua kiuchumi wao wenyewe pamoja na taifa kwa ujumla wake .

Mathias pia amewataka wanafunzi shule za msingi kusoma kwa bidii ili waweze kuondokana na masuala ya unyanyasaji wa kijinsia na kujua kuwa kila mtu anahaki sawa kielimu na kiuchumi.

Kwa upande wa elimu kwa mtoto wa kike alisema , kupitia elimu bora inayotolewa shuleni wanapaswa kusoma kwa bidiii ili waweze kufaulu na kuendelea na elimu ya juu itakayowawezesha kuajiriwa na kujiajiri na hatimaye kujikomboa kiuchumi .

“Ili kwenda na sera ya serikali ya Uchumi wa viwanda vijana mkiwemo wa kike nmapaswa msome kwa bidii ili mweze kutimiza ndoto zenu za kujipatia maendeleo endelevu “ alisema Sidina.

Hata hivyo alitumia fursa hiyo kuwasihi wanafunzi wa shule za msingi kusoma kwa bidiii na pia kuiasa jamii iondokane na unyasasaji wa kijinsia kwa watoto hususani wa kike .

Naye Kiongozi wa HACOCA, Watson Mwankusye alisema, kupitia matamasha yanayoendeshwa na Mashirika yasiyo ya kiserikali , wanawake wanapata elimu mbalimbali ikiwemo ya namna ya kujikwamua kiuchumi kwa kushiriki kuanzisha viwanda vidogo katika maeneo yao.

Hivyo aliwataka wanawake wajiamini zaidi katika kuhakikisha wanajikomboa na kuondokana na dhana ya mwanamke akiwezeshwa anaweza ambayo inawavunja moyo wakati wao wenyewe wanaweza.

Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule ya msingi Azimio `A` Edith Mkude aliwataka wanawake kutumia fursa ya kauli mbiu ya mwaka huu “Kuelekea uchumi wa viwanda, tuimarishe usawa wa jinsia na uwezeshaji wa wanawake vijijini” kufanya kazi kwa bidii kwa kujiunga na vikundi mbalimbali ili kujikwamua kiuchumi.

Mkude alisema kuwa, zama za mwanamke kukaa nyumbani na kutegemea mume zimepitwa na wakati na sasa kunahitajika ushirikiano baina ya mume na mke katika kujenga uchumi wa pamoja kwa ajili ya maendeleo ya familia na taifa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa