• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WANUFAIKA WA TASAF MANISPAA YA MOROGORO WATAKIWA KUTUMIA FEDHA WANAZOPEWA KWA MALENGO YALIYOKUSUDIWA

Posted on: April 6th, 2021

Wanufaika wa TASAF Manispaa ya Morogoro wametakiwa kutumia kwamalengo yaliyokusudiwa fedha inayotolewa kupitia mpango wa kunusuru Kaya masikini unaotekelezwa na mfuko wa maendeleo ya Jamii nchini TASAF.

Rai hiyo imetolewa leo Aprili 06/2021 na Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro , Hilary Sagara, wakati wakizungumza na wanufaika wa mpango huo katika Kata ya Mwembesongo Manispaa ya Morogoro.

Sagara amefanya ziara fupi ya kukagua utaratibu mzima unaotumika wakati wa kugawa fedha hizo na kujionea namna ya wanufaika walivyotoa ushuhuda ni kwa jinsi gani walengwa hao wameweza kubadilisha maisha yao kupitia mpango huo wa kunusuru Kaya masikini.

Amesema kuwa Serikali kupitia TASAF ,imedhamiria kuondoa umasikini wa kipato unaowakabili wananchi wengi nchini na kwamba ili kuunga mkono jitihada za Serikali wananchi ambao ni wanufaika wa mpango huo wanapaswa kutumia fedha hizo kwa kilie kilichokusudiwa.

Amesema kuwa kumekuwa na taarifa kuwa baadhi ya wanufaika wa mpango wa kunusuru Kaya masikini wamekuwa wakitumia fedha hizo vibaya kinyume na malengo yaliyopo huku wengine wakitumia fedha hizo kuongeza wanawake kwa upande wa wanaume na wengine wakitumia kwa ajili ya ulevi jambo ambalo amelipiga marufuku na kuwataka wanaofanya hivyo kuacha mara moja .

Amesema kuwa mpango huo wenye lengo la kupunguza umasikini unatoa fedha hizo kwa ajili ya matumizi ya elimu, afya lakini cha ajabu wananchi wengi mara baada ya kupata fedha hizo wamekuwa wakibadilisha matumizi mazingira ambayo kila siku wamekuwa wakilalamika kuwa fedha hizo hazitoshi.

"Wananchi ni kweli kuwa pesa hazitoshi lakini kwa hiki kidogo mnachokipata ni vyema mkakitumia kwa malengo mazuri mliyojiwekea , haipendezi kuona mtu umepewa pesa ili umpeleke mtoto wako shuleni lakini hufanyi hivyo na badala yake unaenda kutumia kwa ajili ya ulevi, nawahakikishia kwamba Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro tutafanya ukaguzi wa mara kwa mara kuhusu fedha hizi" Amesema Sagara.

Amesema kushindwa kwa baadhi ya wanufaika kuzitumia fedha hizo kwa usahihi ndiko kunakopelekea wananchi kuendelea kuibebesha lawama kila siku Serikali kuwa imekuwa haifanyi kitu chochote cha maana katika kubadilisha pamoja na kuboresha maisha ya Watanzania.

Hata hivyo, amesisistiza kuwa kutoka sasa Kaya ambayo itabainika kutumia fedha wanazopewa kinyume na utaratibu basi upo uwezekano wa kuiondoa ili wapewe wale wenye shida ya pesa ambayo endapo ikitumika vizuri inaweza kubadilisha maisha ya wanufaika.

Naye Kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Morogoro ambaye pia ni Afisa Maendeleo Manispaa ya Morogoro, Enedy Mwanakatwe, amewataka kila mlengwa kutumia fedha hizo vizuri kwa ajili ya kusaidia familia kwa kuwapeleka watoto shule, kliniki na kujiwekea akiba.



Mwanakatwe amesema kuwa fedha wanazopatiwa wanapaswa kuzitumia kwa ajili ya kuboresha maisha yao na kusonga mbele ili maisha yao yawe tofauti na wakati ambapo walikuwa hawajaanza kupata fedha hizo.



Hata hivyo Mratibu wa TASAF Manispaa ya Morogoro, Feliciana Katemana, amewataka walengwa wa TASAF kutumia fedha wanazopatiwa na Serikali kutoka hapo walipo na kwenda ngazi nyingine ambayo itawawezesha kuwavusha kutoka katika umasikini na kupata maendeleo.



"Mnatakiwa kujipima katika kipindi hiki ambacho mmekuwa mkipatiwa fedha, na kujiuliza fedha mlizopatiwa zimewasaidiaje?, wapo walengwa katika kipindi hicho wameweza kufanya mambo makubwa, ni vema mkajiuliza TASAF itakapomalizika utakuwa umepiga hatua gani? '" Amesema Katemana.



Kwa upande wa mnufaika wa TASAF, Hidaya Ramadhani Juma, amesema kuwa fedha hizo za TASAF zimesaidia kupata uhakika wa chakula cha kuwafanya wapate mlo mara tatu na kufanya maendeleo mengine ya kujipatia kipato.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa