• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WAPENDANAO WOMEN GROUP WAKABIDHI SABUNI WODI YA WAZAZI

Posted on: June 30th, 2023

WAPENDANAO WOMEN GROUP WAKABIDHI SABUNI WODI YA WAZAZI MAFIGA

KIKUNDI cha Wakina Mama kijulikanacho kama WAPENDANAO WOMEN GROUP MAFIGA 'A' kutoka Kata ya Mafiga, kimekabidhi msaada wa Sabuni katika Wodi ya Wazazi Kituo cha Afya Mafiga Manispaa ya Morogoro.

Msaada huo umekeabidhiwa Juni 30/2023 kwa Kaimu Mganga Mfawidhi huku Diwani wa Kata ya Mafiga Mhe. Thomas Butabile akiongoza Kikundi hicho pamoja na Viongozi wa Chama na Serikali.

Akizungumza wakati akikabidhi msaada, Mwenyekiti wa Kikundi hicho, Mwanahamisi Juma , amesema wanamshukuru Mwenyezi Mungu wameweza kuwa sehemu ya kupata wasaa wa kutoa msaada huo waliobarikiwa kutoa katika wodi ya Wazazi.

Awali akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo, Kaimu Mganga Mfawidhi wa kituo hicho , Neema Mkuya ambaye pia ni Nesi katika Wodi ya Wazazi, amekishukuru Kikundi hicho kwa kuona umuhimu wa kuwasaidia msaada huo ambao umefika wakati muafaka.

“Nashukuru kupokea neema ambazo mmezileta Wana tupendane,natoa shukrani zangu za dhati kwa ajili ya zawadi na wagonjwa wetu ambao wanajiandaa kupata watoto na wale ambao wameshapata watoto ”Amesema Semkuya.

Mmoja wa wazazi waliopokea msaada wa sabuni, amekishukuru Kikundi cha wakina mama hao na kuwaomba kuendeleza moyo wa kutoa kidogo wanachojaaliwa kusaidia wenye uhitaji.

Naye Diwani wa Kata ya Mafiga, Mhe. Thomas Butabile, amekipongeza Kikundi hicho cha wakina mama kwa masaada wao huku akiomba wadau wengine kujitokeza kutoa misaada kwani Serikali pekee haiwezi kukidhi huduma zote katika kuimarisha huduma ya afya.

Ili kuona Kikundi hicho kinapiga hatua, Mhe. Butabile, amehaidi kuwapa shilingi 200,000/= kwa ajili ya kuongeza mtaji wa Viti kwa kikundi hicho.

“Tunajua msaada huu ni mdogo sana ukilinganisha na mahitaji yaliyopo, lakini tunaamini itasaidia na tunawaomba wengine kujitolea kusaidia kila mmoja kwa uwezo wake, nimeona jitihada zenu na mimi ili kuwaunga mkono nitawapa laki 2 muendeleze mradi wenu wa Viti na katika shughuli zetu nimeagiza Uongozi wa Kata uje kukodi vitu hapa ili tuendelee kuwashika mkono ”Amesema Mhe. Butabile.

Naye Mtendaji wa Kata ya Mafiga, Amina Saidi, amewapongeza wakina Mama hao kwa uthubutu wa kuanzisha kikundi na kujiendesha wenyewe pasipo na mkopo kutoka Serikalini.

Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Mafiga, Mwaru Kizega, amesema katika mikopo ijayo kikundi hicho kinastaili mkopo kwani wameonesha imani kubwa kwamba hata wakipewa mkopo wanauwezo wa kurudisha kwani wameanza miradi na fedha zao jambo ambalo linafaa kuigwa kwa vikundi vyengine.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mafiga A, Ndg. Fadhili Dutilo, ameushukuru Uongozi wa Kata wakiongozwa na Diwani kwa kukubali kuhudhuria katika hafla ya Kikundi hicho huku akiahidi kuendelea kutoa ushirikiano na Vikundi ambavyo vitaanzishwa vyenye lengo la kujikomboa na kujkwamua kiuchumi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa