• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu
        • Msingi
        • Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Ujenzi
      • Afya
      • Maji
      • Mipango, Takwimu, na Usimamizi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Public Relation
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WATENDAJI WA KATA 29 MANISPAA YA MOROGORO WASAINI MKATABA WA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA AFUA ZA LISHE

Posted on: January 25th, 2023

MAAFISA Watendaji wa kata 29 Manispaa ya Morogoro ,wamesaini mkataba wa upangaji, ufuatiliaji na utekelezaji wa shughuli za Lishe kwenye maeneo ya kata zao, huku wakitakiwa kufanya kazi hiyo kwa kuzingatia malengo makuu , viashiria na vigezo vilivyoainishwa kwenye mkataba huo.

Maafisa hao wamesaini mkataba huo baina yao na Mkurugenzi Januari 24/2023 ,katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi Kuu ya Manispaa.

Mkataba huo wa lishe ni hatua ya muendelezo wa uingiaji wa mikataba ya usimamizi wa shughuli za afua za lishe kuanzia ngazi ya Taifa, Mkoa, wilaya na na hatimaye ngazi ya kata na Mitaa .

Akizungumza wakati wa zoezi la utiaji saini mikataba hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro , Fides Likopero, ameweka wazi kuwa, mkataba huo una malengo makuu mawili ikiwa ni kufanikisha suala la kuboresha hali ya lishe na kupunguza athari za utapiamlo na kuhakikisha jamii inashiriki ipasavyo kupanga, kutekeleza na kufuatilia maendeleo ya utekelezaji wa mpango wa halmashauri wa afua za lishe.

Likopero , amesema kuwa kwa kuzingatia malengo hayo Maafisa Watendaji ambao ni wasimamizi wapaswa kufanya kazi hiyo kwa weledi kwa kuzingatia maslahi mapana ya Taifa, kulingana na vigezo na viashiria vilivyoanishwa kwenye mikataba .

"Kila mtu anafahamu umuhimu wa afya bora katika maisha ya binadamu na ujenzi wa Taifa, Serikali imewapa jukumu hili muhimu, nendeni mkalitekeleze kwa umakini mkubwa kulingana na makubaliano, kama kuna changamoto tushirikishane kwa wakati ili kwa pamoja tufikie malengo yaliyokusudiwa na serikali". Amesema Likopero.


Naye Afisa Lishe Manispaa ya Morogoro, Jacqueline Mashurano, amefafanua kuwa, Mkataba wa lishe unawataka Maafisa Watendaji wa Kata kuhakikisha wanashirikiana na Maafisa Watendaji wa Mitaa , kufanya kazi hiyo pamoja na kufanya tathmini na kutoa ripoti ya utekelezaji kwa kila mwezi.

"Lishe duni inanikusababisha umasikini katika Taifa kwani hakutakuwa na Jamii inayoweza kujituma kwa kufanya kazi kutoakana na watu wengi kuathiriwa na utapiamlo, viongozi wenzangu tupambane kutokomeza utapiamlo katika maeneo yetu,ili kuwa na watu wenye afya bora"Amesema Mashurano.

Naye Afisa Mtendaji wa Kata ya Mafiga ,kwa niaba ya Watendaji wenzake, amesema watakwenda kufanyia kazi maelekezo yote kama yalivyo malengo yake kwa kuzingatia vigezo na viashiria vilivyoainishwa kwenye mkata, ikiwa ni pamoja na kuifanya agenda ya kudumu kwenye vikao vyote vya kisheria.


Ifahamike kuwa mkataba wa Lishe ni mkakati wa Kitaifa ambao ulisainiwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan na kusainiwa na Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini.


Matangazo

  • TANGAZO LA UUZWAJI VIWANJA ENEO LA KIEGEA A NA B December 02, 2022
  • ORODHA YA MADEREVA NA WATENDAJI WA MITAA DARAJA LA III WALIOITWA KUFANYA USAILI TAREHE 29/08-1/09/2022 August 22, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI September 06, 2022
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DC NSEMWA AWATAKA WADAU WA SANAA KUCHANGAMKIA MKOPO WA ASIMILI 10 WA HALMSHAURI

    March 10, 2023
  • KATA YA SABASABA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUWAKUMBUKA WATOTO WENYE UHITAJI.

    March 07, 2023
  • MBUNGE MZERU AAHIDI MILIONI 1.5 KUTUNISHA MFUKO WA JUKWAA LA WANAWAKE KIHONDA KUJIKWAMUA KIUCHUMI.

    March 07, 2023
  • DIWANI CHOMOKA KUJA NA MKAKATI WA KUVISAIDIA VIKUNDI KUPATA MASOKO.

    March 06, 2023
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa