• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WATENDAJI WA KATA NA MITAA MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA IBADA MAALUMU YA KUMUOMBEA HAYATI DKT.JOHN POMBE MAGUFULI

Posted on: April 3rd, 2021

Watendaji wa Kata na Mitaa Manispaa ya Morogoro wamefanya ibada maalumu ya kumuombea aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli .

Ibada hiyo maalumu iliyoongozwa na viongozi wa dini mbalimbali, imefanyika leo Aprili 03/2021 kwenye Ukumbi wa Kilakala Soko Kuu la Chifu Kingaru Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza na Waandishi wa habari Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro ambaye pia ni Afisa Tarafa wa Manispaa ya Morogoro, Winfred Kipako, amesema kuwa Hayati Rais. Dkt. John Pombe Magufuli amejenga misingi imara ya uwajibikaji katika utawala bora, na amekuwa mtetezi wa wanyonge katika maeneo mbalimbali aliyopita.

"Tumeshuhudia namna watu wanavyolia juu ya kifo chake, tunapaswa kujifunza namna ya kutumikia wale tuliopewa dhamana ya kuwatumikia katika mambo yao, kikubwa niwaombe sana Watendaji wenzangu tuendelee kujiepusha na matendo ya ukiukwaji wa maadili na kujikumbusha juu ya umuhimu wa kukuza maadili na kuongeza kasi ya kuwatumikia wananchi ili kufikia malengo ya kitaifa na umuhimu wa kuimarisha maadili" Amesema Kipako.

Kipako, amesema kuwa , watu wameguswa na msiba wa Hayati Rais Dkt John Pombe Magufuli, kutokana na mambo mengi aliyoyafanya kwa muda mfupi wa kipindi cha miaka 5 kwenye sekta ya afya sekta ya elimu, maji barabara usafiri pamoja na maendeleo mbalimbali aliyoyafanya .

Aidha, amesema kuwa Tanzania imekuwa na bahati kubwa sana ya miradi mingi ya maendeleo iliyoanzishwa huku akisema imani yake ni kwamba viongozi waliobakia wakiongozwa na Rais wa sasa Mhe. Samia Suluhu Hassan wataifikisha miradi hii katika hatua iliyokuwa imedhamiriwa kufikiwa.

"Watendaji wenzangu huu sio muda wa kujishika tena tayari tumempata Rais mpya mama yetu Samia Suluhu Hassan , Makamu wa Rais Mhe. Philip Mpango, hivyo tukafanye kazi kwa uadilifu wa kiwango cha juu na kuwatumikia Wananchi kwani tunaamini kabisa kila kitu kilichopangwa kitakwenda vizuri kwa sababu mambo ya serikali yanaenda kwa taratibu zake" Ameongeza Kipako.

Akizungumzia swala la kuendelea kufanya ibada kwa ajili ya kumuombea Hayati Magufuli, Mchungaji Thomas Butabile ambaye pia ni Mhe. Diwani wa Kata ya Mafiga , amesema ni vyema kutafakari sisi tuliobaki tumetanguliza nini kwa muumba wetu kila mtu kwa imani yake.

"Kifo ni safari ya wote na kila mtu ataondoka kwa wakati wake, hivyo ni wakati sasa wakushikamana na kujenga upendo wa dhati kwetu sisi tuliobakia ili kuhakikisha kwamba tunatenda yale yaliyomema kwa wananchi wetu na Taifa letu kwa ujumla" Amesema Mchungaji Butabile.

Mch. Butabile, amesema kuwa sasa Taifa limepata Rais mpya Mh. Mama Samia Suluhu Hassani ambaye ni mama mchapakazi, mzalendo mtiifu muadilifu na mtetezi wa wanyonge, hivyo amewaomba Watendaji wa Kata na Mitaa pamoja na Wananchi kuwa na imani na kuendelea kumpa ushirikiano na kubwa ni kuendelea kumuombea kwa Mungu.

"Kazi ya uongozi ni kazi inayohitaji kumtumaini mungu wakati wote, tuendelee kuwapa moyo viongozi wetu na tuendelee kuwaombea kwa mwenyezi Mungu hakuna jambo litakaloshindikana" Ameongeza Mchungaji Butabile.

Naye Sheikh wa Msikiti wa Kingo, Issa Rajabu Issa, amewataka Watendaji , pamoja na Wananchi kuhakikisha wanaishi kwa hofu ya Mwenyezi Mungu huku akisema kuwa wajenga nchi ni mwananchi hivyo amewataka watendaji hao kuwa na ari na bidii ya kujituma ili kufikia malengo waliyojipangia wakiamini kuwa hakuna atakaekuja kujenga Taifa lao bila ya kuanza wao wazalendo na wengine hufuatia .

Mwenyekiti wa Umoja wa Watendaji wa Kata Manispaa ya Morogoro, Bright Sospeter ambaye pia ni Mtendaji wa Kata ya Chamwino, amewataka Watendaji wenzake kuendeleza uaminifu wenye nidhamu na uadilifu katika kutekeleza majukumu ya kazi zao kama Serikali ilivyowaamini kuwakabidhi majukumu hayo.

Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Maafisa Watendaji wa Kata Manispaa ya Morogoro ambaye pia ni Mtendaji wa Kata ya Kilakala, Amina Saidi, ameomba ushirikiano uzidi kuendelea kwa Watendaji wenzanke ili kuweza kuifikisha Manispaa mbele na kuwaletea wananchi maendeleo.

Naye Katibu wa Umoja wa Watendaji wa Kata Manispaa ya Morogoro ambaye pia ni Mtendaji wa Kata ya Mazimbu, Prisca Mawala, amewataka Wananachi kuendelea kutoa ushirikiano dhidi ya Watendaji wao kwani maendeleo yanakuja endapo kuna ushirikiano wa kutosha baina ya Wananahci pamoja na Viongozi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa