• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WATENDAJI WA MITAA WASISITIZWA KUSIMAMIA SHUGHULI ZA LISHE MOROGORO

Posted on: March 25th, 2024

Kikao cha kikazi kati ya watendaji wa mitaa na kitengo cha Lishe cha Manispaa ya Morogoro, kimefanyika leo tarehe 25.03.2024, kwenye ukumbi wa mikutano wa Manispaa hiyo, kwa lengo la kuendelea kuwajengea watendaji wa mitaa uwezo wa usimamizi wa shughuli za Lishe kwenye maeneo yao ya kazi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho ndugu Shaban Dulu, ambaye ni Afisa Utumishi wa Manispaa anayeshughulika na watendaji wa mitaa na kata, amewapongeza watendaji wa mitaa kwa kuendelea kujituma katika utekelezaji wa majukumu yao kisha akawataka watambue kwamba suala la Mkataba wa Lishe ni la kitaifa hivyo kila mmoja wao ahakikishe anasimamia kikamilifu na kwa kiwango kinachotakiwa utekelezaji wake.

“Fahamuni kwamba suala la Lishe liko kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala, ambayo sisi watumishi wa umma ndio watekelezaji wake hivyo nendeni mkasimamie kisawasawa Mkataba wa Lishe, na kila robo taarifa zenu za utekelezaji mziwasilishe kwa viongozi husika wa Manispaa” alisisitiza Dulu.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Lishe Manispaa ya Morogoro ndugu Ester Kawishe, amesema kwa mujibu wa takwimu za kitaifa za hali ya Lishe, Mkoa wa Morogoro bado uko juu katika viashiria vya udumavu, ukondefu na ulishaji wa vichanga na watoto wadogo, huku uzito uliozidi kiasi na kiribatumbo vikiendelea kuongezeka siku kwa siku na kusababisha ongezeko la magonjwa yasiyo ambukiza kama vile saratini, kisukari na mashinikizo ya moyo.

“Wastani wa Serikali wa hali ya udumavu ni asilimia 30, sisi Mkoa wa  Morogoro tuko asilimia 31.8 kwa upande wa ukondefu wastani wa Serikali ni asilimia 3.3 sisi tuna asilimia 3.9, na kwa upande wa ulishaji wa vichanga na watoto wadogo wastani wa Serikali ni asilimia 70 ifikapo mwaka 2025 sisi mpaka sasa tuna asilimia 64” alifafanua ndugu Kawishe.

Ndugu Kawishe amesema hali mbaya ya Lishe na udumavu kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano ndio sababu kubwa iliyopelekea mwaka 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye kwa wakati huo alikuwa ni Makamu wa Rais, kuagiza uwepo wa Mkataba wa Lishe na kuzitaka Halmashauri za Serikali za Mitaa kusimamia utekelezaji wake kuanzia ngazi ya kijiji/mtaa hadi ngazi ya mkoa na kitaifa kwa ujumla.

Hivyo amewakumbusha watendaji wa mitaa shughuli wanazopaswa kuzisimamia katika kuhakikisha utekelezaji wa Mkataba wa Lishe ambazo ni kubandika kwenye mbao za matangazo za Ofisi zao, taarifa za watoto wenye umri chini ya miaka mitano, kuadhimisha Siku ya Afya na Lishe kama mtaa huku wakihamasisha wanaume kushiriki katika masuala ya Lishe, na kuhakikisha wahudumu wa afya ngazi ya jamii wanatembelea kaya na kutoa elimu ya Lishe, Afya, Maji na usafi wa mazingira.

Shughuli zingine wanazopaswa kufanya ni kushirikiana na watoa huduma za afya ngazi ya jamii kufanya ufuatiliaji wa watoto walio acha matibabu ya utapiamlo, na kushiriki katika zoezi la utoaji wa nyongeza ya Vitamin A kwa watoto wenye umri wa miezi 6 hadi 59.

Aidha, kwa mujibu wa takwimu za kadi ya alama (score card) ya upimaji wa utekelezaji wa Afua za Lishe, Manispaa ya Morogoro inaonekana kufanya vizuri kwenye afua takriban zote ikiweo upatikanaji wa chakula kwenye shule za msingi na za sekondari za Manispaa, ambapo inaonesha takriban shule zote za Manispaa zinatoa huduma ya chakula kwa wanafunzi wake.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa