• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WAZIRI JAFO AWATIA MOYO WANAFUNZI SEKONDARI YA KILAKALA.

Posted on: May 20th, 2019

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo amewataka wanafunzi wa Sekondari ya Kilakala Mkoani Morogoro kuendeleza rekodi ya kufanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya kidato cha sita na kuwataka Viongozi wa Mkoa  kusimamia vema ufaulu wa mitihani ya kidato cha nne ili uweze kufanana na ufaulu wa Kidato cha sita au zaidi.

Waziri Jafo ameyasema hayo leo Mei 20 akiwa njiani kikazi kuelekea Mkoani Iringa ambapo alipita katika shule hiyo ya Kilakala na kuongea na uongozi na kisha kuongea na wanafunzi huku akiwatia moyo wanafunzi kufanya vizuri zaidi kwenye mitihani yao.

 “Mimi natamani sana matokeo yenu yakitoka nikiangalia One mmefunga One hapa Kilakala , natamani sana na Mungu awabariki mmpate One ninyi nyote, zingatieni masomo na kuwaheshimu Walimu wenu”amesema Waziri Jafo huku akiwataka viongozi ngazi ya Mkoa na Wilaya kusimamia ufaulu wa Kidato cha Nne katika shule hiyo kwani haujawa mzuri sana kuanzia miaka ya karibuni.

Aidha, Waziri Jafo amesema kwa sasa Serikali ya awamu ya tano chini ya Dt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania inaendelea na ukarabati wa shule 25 kote nchini huku Mhe. Rais akiwa ametoa takribani Sh. Bil2. kwa ajili ya ukarabati huo lengo ikiwa ni kuweka mazingira rafiki ya kujifunzia na kufundishia ili kurudisha umaarufu wa shule hizo kongwe hapa nchini ikiwemo shule ya Sekondari ya Kilakala.

Katika hatua nyingine Waziri Jafo amepokea na kuahidi kulifanyia kazi ombi la Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Bi. Regina Chonjo ombi la kuufanyia ukarabati ukumbi wa Shule ya Kilakala pamoja na nyumba za walimu wanaofundisha shule hiyo ili majengo hayo yafanane na majengo mengine ya shule hiyo ambayo yamekwishafanyiwa ukarabati.

Kwa upande wake Afisa Elimu Mkoa wa Morogoro Mhandisi Joyce Balavuga amemuomba Mhe. Waziri Jafo Jengo, Vifaa na Wataalamu wa masuala ya TEHAMA ili Kuifanya shule ya Sekondari ya Kilakala kuwa kitovu cha Teknolojia Habari na Mawasiliano – TEHAMA kwa ajili ya kuwalea wanafunzi wa shule hiyo kisayansi zaidi Ombi mbalo limepokelewa na Waziri kuwa atalifanyia kazi.

Waziri Jafo kabla ya kuondoka shuleni hapo ametoa ofa ya chakula kwa wanafunzi wa shule hiyo kwa kuwanunulia Mchele kilo 100 na kuku 50 kwa ajili ya chakula, lengo mahususi la Ofa hiyo ni kuwatia moyo wanafunzi hao kusoma kwa bidii ili kufaulu katika mitihani yao na kuleta matunda kwa Taifa la Tanzania.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa