• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WIZARA YA ELIMU YAOMBWA KUANZISHA MCHAKATO MTAALA WA SOMO ELIMU YA MLAJI KWA AJILI YA SHULE ZA MSINGI

Posted on: May 23rd, 2019

Serikali  kupitia Wizara ya Elimu ,Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Tume ya Ushindani (Fair Competition Commission) imeshauriwa kuanzisha mtaala wa somo litakalotoa elimu kwa wanafunzi juu ya kujenga jamii yenye uelewa wa madhara ya matumizi ya bidhaa bandia kutokana na ukuaji wa teknolojia duniani.

Ushauri huo umetolewa na baadhi ya walimu na wanafunzi wa shule ya Msingi Mazimbu A iliyopo katika Manispaa ya Morogoro kuwa kuanzishwa kwa mtaala wa somo hilo kutawezesha siku za usoni kujenga jamii yenye uelewa kwa kuanzia na ngazi ya chini ya familia mpaka ngazi ya juu kielimu .

Mwanafunzi wa shule ya msingi Mazimbu A anayesoma darasa la saba  Irene Materni ,aliiomba Wizara hiyo kuanza mchakato wa kuanzisha mtaala wa elimu ya mlaji kwa ajili ya shule za msingi kwa lengo la kuwawezesha Wanafunzi kupata ulewa wakiwa wadogo ili wanapokuwa wakubwa waweze kukabiliana na changamoto za bidhaa bandia.

Alisema ,amejifunza mambo muhimu katika kukagua uhalisia wa bidhaa ambayo ni ufungashaji wa bidhaa, uandishi wa jina la bidhaa au nembo, usanifu wa mwisho wa bidhaa, bei ya bidhaa ambazo mara nyingi huwa na punguzo la bei, maelezo ya bidhaa ambapo mara nyingi bidhaa bandia hukosa maelezo muhimu.

Naye Mwalimu mkuu wa Shule hiyo, Anitha Nathan alisema , elimu haki na wajibu wa mlaji imetolewa kwa wanafunzi wa darasa la tano na la sita ambapo wao wataifikisha kwa wenzao wakiwa shuleni na kwa wazazi na walezi wao.

Naye Mwalimu Joha Mzuzuri alisema , walimu wa shule tano za msingi Manispaa ya Morogoro walipatiwa mafunzo ya kuwa wakufunzi wa utoaji elimu kwa klabu shuleni kuhusu haki na wajibu wa mlaji.

Mzuzuri alisema ,elimu hiyo iliendelea kutolewa kwa wanafunzi na ni hatua itakayosaidia kukabiliana na changamoto ya ununuzi na matumizi ya bidhaa zisizo na ubora zilizopo katika soko.

“ Walimu wakufunzi wa elimu hii tuliyopata nasi tumeitumia kwa kuwafundisha wanafunzi katika shule zetu ikiwemo ya Mazimbu A kuhusu elimu juu ya haki na wajibu wa mlaji” alisema Mzuzuri .

Mwalimu Mzuzuri alisema ,ili elimu hiyo iwe endelevu kwenye shule za msingi nchini ni vyema Serikali kupitia wizara ya Elimu ,Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na wadau wengine kuanzisha mitaala wa somo hilo.

“ Tukiwajengea uwezo wa elimu wanafunzi wa shule za msingi ni rahisi elimu hii kuwafikia wazazi, walezi na jamii ambayo baadaye inakuwa yenye uelewa kwa kuanzia na ngazi ya chini ya familia mpaka ngazi ya juu kielimu “ alisema Mzuzuri.

Kwa upande wake Ofisa wa Tume ya Ushindani kutoka Idara ya kumlinda Mlaji , Emmanuel Nyanza aliwataka watanzania wawe walalamikaji wenye kuchukua hatua badala ya kunung’unika pasipo kudiriki kuchukua hatua.

Alisema ,endapo watanzania watachukua hatua ikiwa ni pamoja na kuifanyia uchunguzi bidhaa husika na kuifikisha katika vyombo vya kiuchunguzi na kisheria kama vile Tume ya Ushindani nchini (FCC) wahusika wataadhibiwa vikali.

“ Mara nyingi tunanunua vitu na bidhaa mbalimbali bila kuzifahamu au kuzichunguza vyema na hili limesababisha watu wengi kununua bidhaa zisizofaa kwao au zenye madhara kwenye afya zao” alisema Nyanza.

Hata hivyo alisema ,kwa mkoa wa Morogoro Tume hiyo imekuwa ikipokea na kuyafanyia kazi kwa haraka malalamiko ya mlaji pamoja na kuwapa elimu wafanyabiashara.

Nyanza alisema, Tume hiyo iliamua kuanzisha kwenda katika shule za msingi na kuanzisha vilabu za wanafunzi na kutoa elimu ya ulewa wa kumlinda mlaji ili visaidie pia kuelimisha jamii wanapokuwa nyumbani.

“ Tume imeamua kutoa elimu juu ya haki za mlaji kwa kuwa wanafunzi wa kikazi hiki ni kizazi cha kesho ambacho kinapaswa kuwa na ulewa juu ya madhara ya bidhaa bandia “ alisema Nyanza.

Alisema ,kwa hivi sasa Tume hiyo imetoa elimu ya kumlinda mlaji  kwa kuanzia shule tano za Manispaa ya Morogoro ambazo ni Mzimbu A, Kihonda, Mzinga , Kemo na Mafiga ambapo pia imetolewa kwa shule nyingine mkoani Dodoma na na mpango mkakati ni kuifikia mikoa yote hapa nchini.

FCC imeanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Ushindani ya mwaka 2003 na madhumuni makubwa ya uwepo wa Tume ni kukuza na kulinda ushindani wa haki katika biashara na kumlinda mtumiaji wa bidhaa na huduma dhidi ya mwenendo usiofaa katika soko.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa