• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

AFISA AFYA ATETA NA WAHUDUMU NGAZI YA JAMII MOROGORO

Posted on: February 5th, 2024

Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii wa Manispaa ya Morogoro, leo tarehe 05.02.2024 wametakiwa kutoa elimu ya usafi kwenye mitaa yao, sambamba na kufanya tathmini ya hali ya vyoo, na vyanzo vya maji vilivyopo kwenye maeneo hayo hivi sasa ili Manispaa iweze kuchukua hatua za kuhakikisha wananchi wake wanakuwa salama dhidi ya magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu.

Akizungumza kwenye kikao na wahudumu hao, Afisa Afya wa Manispaa ya Morogoro, ndugu Ndimile Kilatu amewataka wahudumu wa afya kutoa elimu hiyo nyumba kwa nyumba huku wakiwasisitiza wananchi kufanya usafi kwenye miji yao na kuweka ndoo zenye koki kwa ajili ya kunawa mikono.

“Kwa wananchi wanaotumia maji ya visima, chemichemi na mito ni lazima wayachemshe kabla ya kuyatumia. Pia hakikisheni mnawapatia wananchi wenu vidonge vya kutibu maji ili waviweke kwenye maji yao ya kunywa” alisisitiza Kilatu.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Manispaa ya Morogoro, Daktari Focus Maneno, amewapongeza wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha wananchi wanapata elimu za afya na kuwataka waendelee kuchapa kazi huku wakifahamu kwamba Serikali inathamini sana huduma yao na inao mpango wa kuirasimisha.

“Tujue kwamba tunalo tatizo la magonjwa ya kuharisha na macho hivyo ni lazima tupite nyumba kwa nyumba tutoe elimu ya afya ili tatizo hili liweze kuisha. Ninyi kwenye jamii mkifanya vizuri na wataalamu wa afya wakafanya vizuri kwenye Zahanati zetu na Vituo vyetu vya Afya, naamini tutatokomeza tatizo hili” alieza Daktari Maneno.

“Lakini elimu mtakayoitoa ni lazima ijikite kwenye miongozo ambayo tumewapatia ili kuepuka uwezekano wa kuzua taharuki miongoni mwa wananchi” alisisitiza Daktari Maneno.

Pia, Daktari Maneno amewataka wananchi kutoogopa kwenda kwenye vituo vya afya endapo watapatwa na ugionjwa wa kuharisha na kutapika hata kama hawatakuwa na pesa, na mara baada ya kupatiwa matibabu na kurudi kwenye makazi yao, wahudumu wa afya wawafuatilie kujua maendeleo ya afya zao.

Nao wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii wamesema wao watapita nyumba kwa nyumba kutoa elimu ya usafi, watahamasisha wananchi waweke ndoo za maji zenye koki kwa ajili ya kunawa mikono na kwa wasio na uwezo wa kununua ndoo hizo watawafunza jinsi ya kutengeneza vidumu chirizi.

Aidha wameuomba uongozi wa Manispia kuhakikisha takataka zinazozalishwa mitaani na kwenye masoko zinazolewa kwa wakati ili kuepuka uchafuzi wa mazingira na magonjwa ya mlipuko pindi mvua zinaponyesha.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa