• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

Posted on: April 12th, 2025

MWENGE wa Uhuru Kitaifa 2025 umezindua miradi ya maendeleo Manispaa ya Morogoro yenye thamani zaidi ya bilioni 1.8 ,ambapo miradi yote imekubaliwa na Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa ,Ndg. Ismail Ali Ussi.

Mwenge huo wa Uhuru Kitaifa mwaka 2025,umekimbizwa Aprili 12-2025 kwa umbali wa Kilometa 91.4 na jumla ya miradi 09 imetembelewa na mwenge huo ambapo miradi 5 imezinduliwa, miradi 3 imeonwa na mradi 1 umetembelewa.

Akizungumza mara baaada ya kukamilika kwa ziara ya kuzindua miradi hiyo ya Mwenge, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, amempongeza Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiletea Manispaa ya Morogoro miradi itakayokwenda kutatua kero za wananchi pamoja na kutoa huduma bora.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Emmanuel Mkongo, amesema miradi hiyo yenye thamani ya shilingi 1,827,898,119.12 , shilingi 542,341,811.45 fedha kutoka Serikali Kuu na shilingi 172,000,000.00 fedha kutoka Mapato ya ndani ya Manispaa, shilingi 130,000,000.00 ni fedha kutoka michango ya wananchi ,shilingi 983,556,307.67 ni michango ya wahisani na Mchango wa Mwenge wa Uhuru ni shilingi 39,600,000.00.

Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Mhe. Abdulaaziz Abood, amesema ataendelea kuhakikisha anazidi kuisemea Manispaa ya Morogoro ili kufikiriwa zaidi katika miradi ya Maendeleo na kutumia nyenzo zake kusaidia maendeleo ili Manispaa ya Morogoro ifikishe adhima yake ya kuwa Jiji.

Naye Meya Manispaa ya Morogoro ,Mhe. Pascal Kihanga, amewashukuru Wananchi wote waliojitokeza katika mapokezi ya Mwenge na kuwataka kuendelea kuwa na imani na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Baraza la Madiwani la Manispaa ya Morogoro.

Miongoni mwa miradi iliyotembelewa na Mwenge ni Ujenzi wa Jengo la Utawala Kola Hill, uliogharimu shilingi 137,000,000.00, Mradi wa kuinua hadhi ya barabara ya Nongeni yenye kilometa 0.72 kwa kiwango cha zege uliotumia shilingi 478,299,123.20, mradi wa nishati safi na salama ya kupikia shule ya Sekondari Morogoro chini ya ufadhili wa EWURA , mradi wa ukarabati jengo la wagonjwa wa nje na ofisi za Utawala, Hospitali ya Mkoa Morogoro kwa gharama ya shilingi 505,257,184.67 kwa ufadhili kutoka Global Fund, mradi wa ujenzi nyumba ya watumishi 2 kwa 1 shule ya Sekondari Konga Mzinga kupitia mradi wa kuimarisha elimu ya Sekondari ( SEQUIP) wenye thamani ya shilingi 95,000,000.00, mradi wa kikundi cha Vijana cha uzalishaji wa mashine mbalimbali ( Hammer Metal Works Group) wenye thamani ya shilingi 35,000,000.00 kupitia mkopoa wa asilimia 10 ya Halmashauri , mradi wa viwanda vidogo vya kutengenezea vipuri (DEBU NG'IMBA FABRICATION WORKS) wenye thamani ya shilingi 70,000,000.00, mradi wa kutengeneza gundi za maji (Vibrant Chemical Company ltd wenye thamani ya shilingi 60,000,000.00, Makao ya Agape ya kulelea watoto wanaoishi mazingira hatarishi na watoto waliofanyiwa ukatili kwa kuwapatia malezi ya familia, na mradi wa ujenzi wa birika la maji lenye ujazo wa lita milioni 1 Mtaa wa nguvu kazi Kata ya Kihonda wenye thamani ya shilingi 61,126,074.55

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • BALOZI BATILDA ATAKA MAONI YA WADAU KUFANYIWA KAZI KUELEKEA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MSHARIKI 2025

    May 06, 2025
  • MAAFISA ARDHI WATAKAOBAINIKA NI VYANZO VYA MIGOGORO YA ARDHI TUTAWAFIKISHA MAHAKAMANI-DKT.NDUMBARO.

    May 05, 2025
  • WAAJIRI SEKTA BINAFSI RUHUSUNI WATUMISHI WENU KUJIUNGA NA CHAMA CHA WAFANYAKAZI - RC MALIMA.

    May 01, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa