• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

CCM YASHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA MANISPAA MORO

Posted on: November 25th, 2019

MSIMAMIZI wa Uchaguzi Manispaa ya Morogoro, Ndg. Waziri Kombo, ametangaza matokeo ya uchaguzi Serikali za Mitaa uliofanyika Novemba 24, ambapo katika matokeo hayo Chama Cha Mapinduzi CCM kimeibuka na ushindi  wa wenyeviti wa mitaa kwa jumla ya mitaa 294.

Akizungumza na Waandishi wa habari Msimamizi wa Uchaguzi Kombo amesema jumla ya nafasi 148 za Wenyeviti wa Serikali za Mitaa wagombea wa CCM walipita bila kupingwa kwakuwa hakukuwa na mgombea wa chama kingine,Mitaa 146 vyama mbalimbali vilichukua fomu za kugombea ila wengine walijiondoa na wengine waliondolewa kwa kukosa vigezo.

Kombo ameeleza kuwa jumla ya Kata 9 na Mitaa 27  ndiyo iliyoshiriki uchaguzi huo baada ya kupita kwa michakato mbalimbali, na kukitangaza chama cha Mapinduzi (CCM) kufanikiwa kuibuka mshindi kwa kunyakua kura zote.

Aidha, amesema kuwa, awali walikuwa na Wagombea 17 wa vyama vya upinzani hivyo walipungua baada ya Viongozi wao wa juu kutoa tamko la kujiengua katika uchaguzi huo na kubakia wagombea wawili kwa upande wa nafasi za Wagombea wa wenyeviti wa Serikali za Mitaa.

Ndg. Waziri akitoa takwimu za matokeo hayo ameeleza kuwa kwa nafasi ya wenyeviti wa mitaa kata ya Uwanja wa Taifa uchaguzi ulifanyika katika mtaa wa Unguu ambapo jumla ya wananchi waliojiandikisha ni 287,idadi ya kura zilizopigwa na vyama vya siasa CCM kura 190,UDP kura 39 na kura moja imeharibika na hii kukifanya chama cha CCM kushinda kwa asilimia 80.Aidha kata ya Mindu uchaguzi umefanyika mtaa wa Kasanga ambapo idadi ya waliojiandikisha kupiga kura ni 789,idad ya kura zilizopigwa na vyama vya siasa CCM kura 448,CHADEMA kura 81,kura tatu zimeharibika na hii imekifanya chama cha CCM kushinda kwa asilimia 67.

'' Uchaguzi umemalizika kwa amani, matokeo kama mlivyo yasikia, chama cha CCM kimeweza kuibuka mshindi na kufanikiwa kuchukua mitaa yote, lakini awali tulikuwa na wagombea wengi wa Vyama vya Upinzani baadae wengine waliondolewa kwa kutokuzingatia kanuni na sheria na wengine walijiengua baada ya matamko ya viongozi wa vyama vyao ''. Amesema Kombo

Amesema kwa upande wa Wagombea nafasi za Wajumbe Mchanganyiko kulikuwa na nafasi za wagombea 882 na upande wa Wagombea Viti Maalumu Wanawake nafasi zilikuwa 588 katika Kata zote na nafasi ya wenyeviti wa mitaa nafasi zilikuwa 2kwa  Mitaa yote ambayo uchaguzi umefanyika.

Miongoni mwa Vyama vilivyoshiriki katika uchaguzi huo ni pamoja na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), United Democreatic Party (UDP),Chama cha Mapinduzi(CCM) na Civic United Front(CUF).

Aidha, amewapongeza Wananchi waliojitokeza katika uchaguzi huo na kufanikisha uchaguzi kumalizika kwa amanai pasipo na uvunjifu wowote wa sheria.

Pia amewapongeza sana Wasimamizi wa uchaguzi kwa kusimamia vyema uchaguzi huo kwa kufuata misingi ya haki, huku akitoa rai kwa Viongozi waliochaguliwa waende kuwatendea haki wananachi wao kwa mustakabadhi wa maendeleo ya Taifa na Wananchi wao .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa