• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC CHONJO AIUNGA MKONO TAASISI YA WILDNA FOUNDATION KWA KUWAPA KIASI CHA SHILINGI MILIONI MOJA KWA AJILI YA KUWASAIDIA WANAWAKE WANAOISHI KATIKA NYUMBA ZA POLISI MANISPAA YA MOROGORO

Posted on: March 19th, 2020

MKUU wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo, ametoa kiasi cha Shilingi Milioni Moja 1,000,000/= kama ahadi aliyoiahidi kwa Taasisi ya Wildina Foundation inayojishughulisha na kuwasaidia kuwanyanyua kiuchumi pamoja na kuwaendeleza wakina Mama wanaoishi katika nyumba za Polisi Manispaa ya Morogoro inayoongozwa na Mama Yustina Mutafungwa ambaye ni mke wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro .

Hafla hiyo fupi ya kuwakabidhi fedha hizo ikiwa ni njia ya kuwaunga mkono wakina Mama wanaoishi katika Nyumba za Polisi Manispaa ya Morogoro, imefanyika leo Machi 19, 2020 Ofisini kwake.


Akizungumza na Waandishi wa habari, DC Chonjo, amesema kuwa ametoa kiasi hicho cha fedha kama ahadi yake kufuatia kuwaahidi katika mkutano walimualika wa harambee ya kuchangia fedha kwa ajili ya kupata mtaji wa kuendeleza Taasisi hiyo ikiwa na lengo la kujikwamua kiuchumi.



“Natoa fedha mimi nikiwa Mkuu wa Wilaya hii ya Morogoro,najua Taasisi hii imekuwa msaada mkubwa kwa wakina Mamam hapa mkoani Morogoro bila kusahau mimi pia Mwanamke mwenzao , fedha hizi ni ahadi yangu kwenye harambee waliyonialika , lakini natarajia kuona fedha hizi zitakwenda kutunisha mfuko wenu wa uwezeshaji wa kiuchumi wa wakina mama, natambua kwamba wakina mama ambao ni wake wa Polisi ni ndugu zetu na hawa ndio ambao wanawalinda Askari zetu wanaolinda usalama wa raia na mali zao, kwahiyo wanapokuwa na jambo lao lazima sisi Viongozi tuwaunge mkono, maana kukiwa na maugovi na mapungufu katika Familia hata hawa askari wetu wanakosa hali ya kutulinda sisi Wananchi, tunafahamu hali zetu katika mishahara ”Amesema DC Chonjo.



Aidha amesema kitendo cha kuundawa kwa Taasisi hiyo kumetokana na kujiongeza kwa Wakina Mama kwani wengi wao wanafamilia hivyo wameona ni vyema wakajiingiza katika shughuli za Ujasiriamali kwa kuuza Chakula, Mapambo , Ushonaji wa Nguo, ushonaji wa Vikapu na mikeka pamoja na kufanya shughuli nyengine ili waweze kujikomboa na kuacha utegemezi na kuzilea familia zao zikaaishi maisha bora.



Amesema kutokana na juhudi walizozionesha zilimfanya kuwaunga mkono ili waweze kufanya shughuli zao za kuongeza kipato katika Familia ukizingatia wao ni wakina Mama kama alivyo yeye na anategemea baadaye kuwaona wakiwa na maisha mazuri huku wakitembea kifua mbele.



Pi amesema kuwa hatua waliyofikia ni madhubuti ya kujenga uwezo wa wanawake waweze kujitegemea ili waweze kufanya maamuzi juu ya maisha yao na kutekeleza maamuzi hayo kwa kutumia rasilimali zilizopo bila kuingiliwa au kubughudhiwa na mtu, taasisi au chombo chochote kwa sababu tu, wao ni wanawake.



Naye Mwenyekiti wa Wildina Foundation, Bi. Yustina Wilbrod Mutafungwa, amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa upendo na moyo aliouonyesha kwa kuwakabidhi ahadi aliyoiahidi katika harambee waliyomwalika.



Amesema kuwa, mchango wake hautaenda bure, bali watautumia kwa malengo waliyokusudia ili kuweza kusongesha gurudumu mbele la kuongeza kipato katika familia za wakina mama wanaoishi katika Kambi na nyumba za Polisi.



“Tunamshukuru sana Mama yetu Chonjo, amekuwa mstari wa mbele sana kusaidia jitihada zinazofanywa na Jeshi la Polisi ukizingatia naye aliolewa na askari, hivyo kama Mwanamke na Mama mwenzetu amekuwa ni mtu wa karibu sana kwetu , kila tunapopata jambo tukimwambia amekuwa mtu wa maamuzi na kutusaidia alituahidi na leo ametekeleza lakini kwa hili la leo tutamuhakikishia kwamba tutarudi Ofisini kwake tukiwa kifua mbele kabisa kwa mafanikio tutakayoyapata kikubwa aendelee na Moyo huo huo na asituchoke pale tutakapokuwa tumekwama “Amesema Mama Mutafungwa.



Amesema lengo la kuanzisha Taasisi hiyo ni kuweza kuwanyanyua wakina Mama na wanawake wanaoishi katika Nyumba za Polisi kwani wengi wao wanaishi katika mazingira magumu na hawawezi kufanya kazi na vipato vyao ni vidogo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa